Pages

Tuesday, May 14, 2013

MASKINI ANGELINA JOLIE AKATWA MATITI YAKE NA KUONDOA MFUKO WAKE WA UZAZI







 MCHEZAJI wa filamu mashuhuri sana duniani,Angelina Jolie amesema kwamba amekatwa matiti yake yote pamoja na kuondoa mfuko wake wa uzazi.

Kwenye taarifa aliyoandika kwenye gazeti la New York Times, Bi Jolie amesema alifanyiwa uchunguzi wa celi zake na kugunduliwa kwamba alikuwa katika hatari kubwa sana ya kupata saratani ya matiti. Ndipo akaamua kukatwa matiti yake mawili.

Angelina mwenye umri wa miaka 37 na mama na watoto sita, alipoteza mamake mzazi kutokana na maradhi ya saratani ya matiti.

Anasema aliandika taarifa hiyo kuwahakikishia watoto wake kwamba hakuwa kwenye hatari ya kupata saratani tena.

Kulingana na Jolie madaktari walisema kuwa uwezekano wake kupata Saratani ya matiti ni asilimia 87 huku akiwa na asilimia 50 uwezo wake wa kuugua Sarati ya mfuko wa uzazi.

''Niliamua kuchukua hatua mwenyewe ili kuzuia uwezekano wowote wa kuugua Saratani hiyo,'' alisema Jolie.

Alisema kuwa shughuli hii ilianza mwezi Februari na kukamilika mwishoni mwa mwezi April.
Katika taarifa iliyoandikwa na Bi Jolie na yenye kichwa, 'Uamuzi wangu wa kimatibabu', Bi Jolie alieleza kuwa mamake alipambana na Saratani kwa miaka kumi na kufariki akiwa na umri wa miaka 56.


Alisema kuwa alielewa fika kuwa siku moja atawahi kuugua Saratani na ndio maana akachukua uamuzi wa kufanyiwa upasuaji huo mgumu wa wiki tisa ambao ulihitaji kukatwa matiti.

Uwezekano wake wa kuugua saratani sasa umeshuka kutoka 87% hadi 5%.
Alimsifu mumewe Brad Pitt, kwa kumuunga mkono na kumfariji kwa kila aliyopitia, na kusema kuwa ametulizwa na kuwa wanawe hawakupata lolote katika matokeo ya uchunguzi wa madaktari tangu kufanyiwa upasuaji.


"ninahisi kuwa na nguvu kwa uamuzi niliofanya, na kwa kuwa ninasalia kuwa mwanamke hata baada ya kuondoa viungo hivyo,'' alisema Bi Jolie.

"kwa mwanamke yeyote anayesoma maneno haya, natumai ataweza kujua kuwa wanaweza kufanya uamuzi.''

Muigizaji huyo, ambaye ameshinda tuzo nyingi kwa uigizaji wake, pia ni mtunzi wa filamu na mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa anayehusika na harakati za kibinadamu.

Wakati alipokuwa anafanyiwa upasuaji, Bi Jolie alizuru Jamuhuri ya Kidremokrasia ya Congo pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague.

Friday, May 10, 2013

WAENDESHA DALADALA WAGOMA KUSAFIRISHA ABIRIA LEO MJINI IRINGA



 mmoja wa madereva wa daladala akiwatuliza madeveva wenzie
Ofisa  wa  Sumatra  mkoa  wa Iringa Rahim Kondo





usafiri uliotumika leo kubeba abiria

Mgomo  wa  daladala katika Manispaa ya Iringa umeanza asubuhi hii katika eneo la Mwang'ingo mjini Iringa kwa  madereva na   wamiliki   wa  daladala mjini hapa kudai  kuchoshwa na manyanyaso ya afisa mpya  wa SUMATRA mkoa  wa  Iringa.
Habari  ambazo  mtandao huu umezipata zinadai  kuwa hatua ya  mgomo huo  imekuja   kutokana na kuchukizwa  uamuzi  wa Sumatra  mkoa  wa Iringa  kufuta  stendi ya  posta pamoja na  kuzuia daladala  kukaa kwa muda  eneo la stendi ya  daladala  ya Miyomboni maeneo ambayo  kimsingi  walikuwa  wakikaa siku zote. 
Madereva  hao  wamesema  kuwa leo  hawapo   tayari  kufanya kazi hadi  hapo afisa  huyo  wa Sumatra  mkoa  wa Iringa atakapofuta maagizo yake ya  kuzuia stendi hiyo ya  posta na kuruhusu daladala  kukaa muda zaidi  eneo la Miyomboni.

Hali  hiyo  imeanza  kutikisha  na kufanya  polisi  kuingilia kati  kuwatuliza  madereva  wasigome jitihada  zinazoendelea  hadi  sasa.

Hata  hivyo usafiri  unaofanya kazi ni bajaji  ,pikipiki na Taxi ambapo nauli  kwa kichwa katika bajaji  Tsh. 3000 wakati Taxi kwa kila kichwa Tsh 1000

Wednesday, May 8, 2013

Hatimaye Lwakatare afutiwa kesi ya ugaidi!




BREAKING NEWS!
 
 Lwakatare afutiwa Kesi ya Ugaidi!
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Wilfed Lwakatare.

Mahakama Kuu ya Tanzania imefuta mashtaka yote ya ugaidi yaliyokuwa yanamkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Wilfed Lwakatare.

...
Taarifa kutoka Mahakama Kuu zinasema Mahakama Kuu imebakiza shitaka moja tu, la utekaji ambalo kimsingi ni Jinai na lina dhamana.

Taarifa zaidi zinasema ni shangwe kuu kutoka kwa wafuasi wa Chadema walioko mahakamani na Familia ya Lwakatare.Baadhi ya wafuasi wa Chadema waliohojiwa wamesema huu ni ushindi mkubwa dhidi ya udhalimu.

Katika kesi hii Lwakatare anawakilishwa na Jopo la mawakili nguli watano ambao ni Mabere Marando, Tundu Lissu, Professor Abdallah Safari, Peter Kibatala na Naronyo Kicheere.

Chanzo Kutoka Mahakamani.

Monday, May 6, 2013

MWANAMKE AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MAJAMBAZI




AMEUAWA KWA KUPIGWA RISASI KIFUANI NA MAJAMBAZI JIJINI DAR'

'Majambazi yamempora mama mmoja kiasi cha shilingi milioni kumi na kutokomea nazo kusikojulikana....
Tukio hilo limetokea jana saa 5:16 jioni na


Inavyosemekana ni kuwa mwanamke huyo alikuwa akitoka benki ya CRDB tawi la Uhuru ambapo majambazi yakiwa na pikipiki yalikuwa yakimfuatilia..
Alipotoka ,majambazi hayo yalimfuata na kuligonga gari lake makusudi na ndipo dada huyo aliposimama ili kuangalia nani kagonga gari yake ambapo jambazi mmoja alishuka na kumpiga risasi ya kifuani na kutokomea na kiasi hicho cha pesa. ..

MILIPUKO KANISANI JIJINI ARUSHA





JESHI  la polisi jijini Arusha limesema linamshikilia mtu mmoja kwa tuhuma za kuhusika katika tukio la ulipuaji lililofanyika katika kanisa la Arusha.

Tukio hilo ambalo limetokea majira ya saa tano asubuhi ya leo tarehe 5 mwezi huu Mei  katika Parokia ya Mpya ya Joseph Mfanyakazi iliyokuwa inafunguliwa rasmi kumetokea mlipuko uliojeruhi watu zaidi ya 25.

Parokia hiyo teule ya orasiti- ya mtakatifu Joseph mfanyakazi Arusha ilikuwa ikifanya uzinduzi mpya, ambapo Kwa mujibu wa taarifa zinazosikika moja kwa moja kupitia Radio Maria, Tanzania, mlipuko huo umetokana na kitu kinasadikika kuwa ni bomu.

Hata  hivyo haijafahamika ikiwa mlipuko huo ulikuwa niwa  bomu la kutegwa ama la kurushwa kwa mkono kutokana na jeshi la polisi kuendelea na uchunguzi wake juu ya mlipuko huo.

Inaripotiwa kuwa wengi wamejeruhiwa miguuni na kulazimika kuwahishwa hospitalini kwa matibabu zaidi. Hakuna taarifa zozote za kifo zilizoripotiwa katika tukio hilo.

Aidha viongozi mbalimbali wa Kanisa akiwemo mwakilishi wa Papa aliyekuwa anatabaruku Kigango hicho kilichozaliwa mwaka 2008 kuwa Parokia, Padre Francisco Padilla na viongozi wa jeshi la polisi na usalama, wanaendelea na kikao ili kuamua hatima ya misa iliyokatizwa.

Hata hivyo kutokana na usalama wa waumini waliokuwemo katika kanisa hilo, wametakiwa kuondoka na hivyo kukatishwa kwa misa na matukio hayo ya uzinduzi.

Viongozi mbalimbali wa mkoa wa Arusha, akiwemo mkuu wa mkoa, Mbunge wamefika katika eneo hilo, huku jeshi la polisi likiendelea na uchunguzi

Monday, April 1, 2013

JENGO LILILOANGUKA DAR WALIOKUFA SASA NI 29!!




Maghorofa matatu watu wahamishwa
  Mkandarasi diwani wa CCM mbaroni

Wakati miili ya watu waliokufa katika jengo la ghorofa 16 lililoporomoka Ijumaa ya wiki iliyopita jijini Dar es Salaam iliyopatikana ikiwa imefikia 29, serikali imeamuru watu waliopo katika maghorofa mengine matatu yaliyopo jirani na ghorofa hilo kuhama mara moja kwa sababu hayapo katika hali ya usalama.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema majengo hayo yanayomikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wapangaji wake wanatakiwa kuondoka ili uchunguzi ufanyike kubaini kama yana uimara unaotakiwa.


Sadiki alisema majengo hayo yanaweza yakawa yamepata mtikisiko mkubwa kutokana na kuwa karibu na ghorofa lililoanguka na ghorofa moja kati ya hayo matatu tayari limeonyesha dalili za kuwa na nyufa.

“Nimewaagiza Shirika la Nyumba la Taifa kuwaondoa wapangaji wake wote waliopo karibu na ghorofa lililoporomoka ili uchunguzi wa majengo hayo ufanyike,” alisema Sadiki.
Alisema NHC watagharamia gharama zote za mazishi kwa maana ya jeneza, sanda na kusafirisha miili ya waliokufa kupelekwa katika maeneo mbalimbali ya nchi.

WALIOKUFA WAFIKIA 29
Awali akizungumza na NIPASHE jana mchana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema kuwa idadi ya watu waliokufa imefikia 28.

Hata hivyo, baadaye jioni Sadiki aliiambia gazeti hili kuwa idadi hiyo imeongezeka na kufikia watu 29 na kwamba hadi saa 1:10 usiku zoezi la kutafuta miili zaidi lilikuwa linaendelea.

Sadiki alisema zoezi hilo litaendelea ili kuhakikisha kwamba linakamilika kwa siku ya jana.

WALIOKAMATWA WAONGEZEKA
Katika tukio lingine; Kamanda Kova alisema kuwa idadi ya watu wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kuhusiana na tukio hilo imeongezeka na kufikia wanane.

 Aliwataja wanaoshikiliwa kuwa ni mmiliki wa ghorofa hilo, Raza Husein Damji (69) na mtoto wake, Ally Raza Damji (31) ambaye alikuwa akishirikiana naye.

Wengine  ni wafanyakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala,  Mhandisi Ogare Salu, Mhandisi wa Majengo , Goodluck Mbagaga, na Mkaguzi wa Majengo, Wilbroad Mugyabusu.

Mkandarasi wa Kampuni ya Lucky Construction iliyokuwa ikijenga jengo hilo na ni Diwani wa Goba (CCM) katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Ibrahim Mohamed Kisoki.

Pia wamo  Zonazea Anage Oushadada (53), ambaye ni Mhandisi Mshauri na Mohamed Abdulkarim (61), mshauri wa kujitegemea aliyekuwa akitumiwa na mmiliki wa jengo.
Alisema watu waliokamatwa kuhusiana na tukio hilo kama wangekuwa makini, janga hilo lisingetokea na kwamba wakati wakiendelea kuhojiwa, Jeshi la Polisi nalo litaendelea kuchunguza.

Kova alisema wakati wa zoezi la kuokoa watu waliofukiwa na kifusi cha jengo hilo likiendelea, walikuta nondo na mifuko kadhaa ya saruji ambayo ilikuwa imefukiwa kabla ya kutumika.

 Alisema kutokana na tukio hilo, serikali imemua kuchukua majina ya watu ambao ni wataalam wa masuala ya majanga ili kunapotokea janga wanaitwa haraka kusaidia.
 Kamanda huyo alitoa onyo kwa watu wanaochukua nondo zinazotupwa pamoja na kifusi kutoka katika jengo lililoporomoka na kwenda kuziuza na kwamba wakikamatwa watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

‘MAGHOROFA YOTE DAR ES SALAAM SIYO SALAMA’
Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia, akizungumza jana na waandishi wa habari, alisema majengo mengi hususani maghorofa katika Jiji la Dar es Salaam siyo salama kwa kuishi.

Mbatia alisema majengo hayo siyo salama kutokana na kujengwa chini ya kiwango na kwamba kama kukitokea tetemeko la ardhi, majanga yanaweza kutokea kila wakati.

Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, alisema kutokana na hali hiyo, serikali inatakiwa kuchukua maamuzi magumu kuwaondoa wananchi wanaoishi katika maghorofa na kufanya utafiti wa majengo hayo kubaini kama yana uimara unaotakiwa.

“Vifaa vya ujenzi TBS (Shirika la Viwango la Taifa) linapitisha tu, pia wapo watu wanaotoa vibali nao wanatoa vibali tu bila kufanya utafiti na kufuatilia ujenzi wa maghorofa, hii ni hatari katika nchi yetu,” alisema Mbatia.

Mbatia ambaye ana taaluma ya uhandisi alisema: “Yametokea matukio mengi ya maghorofa kuporomoka, lakini bado  hatujajifunza na  tukio hili lililotokea mfano likijitokeza jingine hili lililotokea litasahaulika.”

Alisema kuna haja ya kuwa na kitengo maalum cha kushughulikia majanga na wabunge katika mkutano ujao wa Bunge wanatakiwa kushinikiza suala hilo.

Naye Mbunge wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi), Moses Machali, alisema ghorofa pacha na lililoporomoka lililokuwa likijengwa na mkandarasi mmoja linatakiwa kubomolewa haraka ili lisije likasababisha janga jingine.

“Serikali ilibomoe haraka jengo hili na kama haitatekeleza tutajua kuna mkono wa rushwa, tunahitaji kuona nguvu ya John Magufuli (Waziri wa Ujenzi) kama masuala ya ujenzi wa majengo siyo kwenye ujenzi wa barabara tu,” alisema Machali.
Machali alisema kama jengo hilo halitaangushwa, watatangaza mgogoro na serikali.

WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI KUTOA TAMKO

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye, alisema wizara yake itatoa tamko la serikali baada ya kazi ya kufukua kifusi cha ghorofa hilo lililoporomoka kukamilika.

Medeye alisema utata kuhusu kibali kilichotolewa kama kilikuwa cha kujenga ghorofa tisa au 16 litatolewa ufafanuzi.

KIKWETE ATEMBELEA WAJERUHI MUHIMBILI

Rais Jakaya Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete jana waliwatembelea majeruhi wa ajali ya  jengo lililoporomoka hivi karibuni waliolazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Rais Kikwete aliyeambatana na mkewe, Salma na  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sadiki, alifika MNH majira ya asubuhi kwa ajili ya kuwajulia hali majeruhi hao.

Alitembelea wodi ya Sewahaji namba 17 walikolazwa majeruhi wawili, pamoja na Taasisi ya Mifupa (Moi) katika wodi binafsi ya  wagonjwa walikolazwa wengine wawili.

Akizungumzia tukio hilo juzi, Kova alisema zoezi ya uokoaji liliendelea usiku kucha na miili hiyo imehifadhiwa MNH ilikowekwa kambi itakayosaidia watu kugundua miili ya ndugu zao.