Pages

Tuesday, December 31, 2013

WAFANYABIASHARA MWANZA WAZIGOMEA MASHINE ZA KIELETRONIKI (EFD)

"HATA BURE HATUZITAKI"

Shughuli za biashara ya maduka na huduma mbalimbali za kijamii katika jiji la Mwanza zimesimama kwa siku nzima kufuatia mgomo wa wafanyabiashara wakubwa na wa kati zaidi ya 2000, wanaopinga matumizi ya mashine za kodi za kielektroniki-EFD .

Ni sauti za wafanyabiashara wa jiji la Mwanza, wakiwa wamekusanyika katika kituo kikuu cha zamani cha mabasi cha stendi ya Tanganyika,

 kilichopo katikati ya jiji la Mwanza, huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe unaoelezea namna wanavyonyanyasika kutokana na matumizi ya mashine hizo

Baadhi ya wafanyabiashara wakizungumza kwa jazba, wamesema hawako tayari kufanya biashara kwa kutumia mashine za TRA, hata kama watapewa bure kwa madai kwamba wengi wao bado ni wajasiriamali ambao mitaji yao bado ni midogo, huku wengine wakidai kwamba TRA haijawapa elimu kuhusu matumizi ya mashine hizo zaidi ya kuwapa muda wa kuanza kuzitumia



Mgomo huo, ambao umeathiri maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza na kusababisha usumbufu mkubwa kwa baadhi ya wakazi wa mikoa ya kanda ya ziwa, wanaotegemea kununua bidhaa mbalimbali kutoka katika maduka ya jumla yaliyopo jijini Mwanza, umemlazimu meneja wa mamlaka ya mapato ( TRA ) mkoa wa Mwanza Bw. Jeremiah Lusana pamoja na kaimu katibu tawala wa mkoa wa Mwanza Bw. Ndaro Kulwijila kuutolea tamko.


Via ITV

Friday, December 27, 2013

BREAKIN NEWZZZ!!- PICHA ZAKWANZA ZA THIS SUPER STAR MODEL MBONGO KUKAMATWA NA SEMBE MACAO/CHINA

Heroin drug packer arrested in Macao (2013-12-19) 
A woman from Tanzania was arrested on  a charge of drug possession in Macao, Dec 19, 2013. Police officers became suspicious of a female passenger who had flown from Thailand to Monaco on Tuesday (Dec,17,2013). The suspect, a tanzanian National, 28 was allegadly trying to smuggle drugs into Guangzhou. Guangzhou Proivence. After undergoing an X-ray scan, the suspect excreted 66 pellets of heroin, weighting 1.1 kilograms valued 1.1 millionMacao pataca ($137,755)







SUPER STAR DIAMOND PLATZNUM ALIPOMTANGAZA RASMI MCHUMBA WAKE MUPYA JANA LIVE!!


Ilikuwa jana pale Leaders club kwenye show ya Diamond ambapo Wema Sepetu alipanda kwenye stage na kuongea na mashabiki waliofika kwenye show hiyo.
Kwenye hiyo show Diamond aliuliza,”Mnataka kumjua mchumba wangu”?
Show ilivyoendelea Diamond alitaka kuimba wimbo wa ukimwona akasema, “Naskia ninayetaka kumuimbia wimbo huu yupo humuhumu ndani”.
Wema Sepetu akapanda kwenye stage wakaimba na kucheza wote.







Friday, December 20, 2013

MKALIMANI WA LUGHA YA ISHARA KATIKA SIKU YA MAZISHI YA MANDELA ALAZWA HOSPITALI YA MAGONJWA YA AKILI


MKALIMANI WA LUGHA YA ISHARA KATIKA SIKU YA MAZISHI YA MANDELA ALAZWA HOSPITALI YA MAGONJWA YA AKILI

Mkalimani huyo anashutumiwa kutoa ishara ambazo hazikuendana na kile kilichokuwa kikiongelewa.
Thamsanqa Jantjie “anaweza kuwa na matatizo”, amekaririwa mke wake Siziwe akisema hayo.
Wataalam wa lugha ya ishara wamemshutumu kwa kutoa tafsiri potofu wakati viongozi mbalimbali wakitoa hotuba zao kwenye mazishi ya kitaifa ya Bwana Nelson Mandela wiki iliyopita.
Bwana Jantjie amesema aliumwa ghafla ugonjwa wa schizophrenia.
Amesisitiza kuwa alikuwa ni mkalimani mwenye ujuzi wa kazi hiyo.
Chama tawala cha African National Congress,ANC, amesema imekuwa ikimtumia Bwana Jantjie kama mkalimani wa lugha ya ishara katika matukio kadha siku za nyuma na hakuwahi kulalamikiwa kuhusiana na huduma yake, kwa upande wa ujuzi au maradhi yoyote.
Bwana Mandela alifariki dunia tarehe 5 Desemba mwaka huu akiwa na umri wa miaka 95 na kuzikwa Jumapili.

via Kibs 24

Tuesday, December 17, 2013

WASICHANA WAWILI WADAKWA NA DAWA ZA KULEVYA UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU NYERERE



Kamanda Godfrey Nzoa

Polisi imewakamata wasichana wawili wa Kitanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam, wakiwa na zaidi ya pipi 187 za madawaya kulevya   walizokuwa wamezimeza  kwa ajili ya kusafirisha nchini China.

Aidha, polisi imemtia mbaroni, raia wa China Guoyn Shen (44), kwa kukutwa na madini aina ya quates kilo 19 aliyokuwa akiyasafirisha kwa njia ya ndege kuelekea China.


Wasichana waliokamatwa Jumatano ya wiki hii saa 11:00 jioni. uwanjani hapo walikuwa kwenye harakati za kupanda ndege ya kampuni ya ndege ya Qatar kuelekea China kupitia Hong Kong.

Kwa mujibu wa Mkuu wa kitengo cha kupambana na dawa za kulevya, nchini Kamanda Godfrey Nzoa, wasichana hao ni Mariam Makuhani (29) mkazi wa Tabata Kimanga  na Khadija Shomari (30), mkazi wa Magomeni Mapipa ambao hadi jana asubuhi walikuwa wanaendelea kuzitoa pipi hizo kwa njia ya haja kubwa.
Alisema Mariam kwa wakati huo (saa 5:00) alikuwa ametoa pipi 65  wakati Khadija alifanikiwa kutoa pipi 122 ambazo zitapelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kubaini ni za aina gani na thamani yake.

Alisema wasichana hao bado wapo chini ya uangalizi ambapo baada ya kumaliza zoezi hilo wataandaliwa mashitaka yao na kufikishwa mahakamani kujibu makosa yanayowakabili.

Kaimu wa Viwanja vya Ndege nchini, Mratibu wa polisi, Renatus Chalya, alisema awali baada ya wasichana hao kukamatwa, Mariam alikiri kumeza pipi 72 huku Khadija akidai alimsindikiza Mariam.


Akizungumzia changamoto za kupambana na madawa ya kulevya, Kamanda Nzoa alisema wasafirishaji wamekuwa wakiibuka na mbinu tofauti na wengine wakisafirisha viatilifu vya kutengenezea dawa hizo badala ya dawa zenyewe.

Alisema mbinu hizo zimekuwa zikifanywa kwa msimu na kutaja njia ambazo hutumiwa kuwa ni majini, viwanja vya ndege na nchi kavu.

Kufuatia changamoto hiyo, Tanzania na nchi nyingine duniani zilishiriki mikutano mbalimbali ambapo wa mwisho ulifanyika mwezi Oktoba mwaka huu nchini Afrika Kusini.

Alisema katika mkutano huo washiriki pamoja na mambo mengine walipata fursa ya kueleza changamoto wanazokabiliana nazo kwenye mapambano dhidi ya dawa hizo ambapo lililojitokeza ni usafirishaji wa viatilifu.


"Tuliliongelea kwa upana wake suala hili na kuafikiana kuwepo kwa sheria kali kwa kuwa tunayoitumia kwa mfano Tanzania haiwabani sana," alisema na kuongeza:
Alisema nchi zilizoshiriki mkutano huo zilibaini hiyo ni moja ya changamoto hivyo wakakubaliana kutungwe sheria itakayokuwa na makali zaidi.


Kamanda Nzoa aliwataja Watanzania wawili waliokamatwa kwa nyakati tofauti na viatilifu Agnes Masogange, Afrika Kusini na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Sada  aliyekamatwa Tanzania ambao kutokana na sheria hiyo walilipa faini ndogo na kuachiwa huru.


Alisema sheria iliyopo inatoa nguvu kwa mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ambapo mtu akikamatwa na viatilifu hivyo bila kibali atachukuliwa hatua za kisheria.
Kamanda Nzoa alisema kuanzia mwezi Machi hadi Julai mwaka huu, wamefanikiwa kukamata kilo 1482 ambazo tayari zilishaharibiwa.


Alisema dawa hizo zilikamatwa kwa nyakati tofauti kwenye meli ambapo moja ilikutwa na kilo 500, nyingine kilo 300.

"Ipo iliyokutwa na kilo 200 meli nyingine ilikutwa na kilo 182 ambapo hata hivyo kutokana na eneo walilokutwa walishindwa kuwafikisha mahakamani badala yake waliharibu mzigo huo," alisema.

Kwa upande wa njia ya anga, alisema kwa mwaka huu wamefanikiwa kukamata kilo 50 bila kuzijumlisha zinazoendelea kutolewa na wasichana hao wawili waliokamatwa Jumatano.

"Ipo kesi ambayo ukija hapa ofisi kwangu nitakuonyesha mlolongo mzima, huwezi amini tulikamata watu tena wakazitoa dawa hizo kwa njia ya haja kubwa lakini mahakama iliwaachilia, kama nilivyosema tunapoenda mahakamani tunatakiwa kuthibitisha pasipo kuacha shaka," alisema.

Kamanda Nzoa alisema kutokana na changamoto hizo, tayari wameshawapeleka vijana wao nchi mbalimbali na kutaja baadhi kuwa ni Afrika Kusini, Ghana, India, Iran, Ivory Cost  kwa ajili ya mafunzo maalum.

Kuhusu Mchina aliyekamatwana madini alisema kuwa Shen alikamatwa Jumatano wiki hii uwanjani hapo akiwa kwenye harakati za kusafirisha mzigo huo kuelekea nchini humo.

Alisema mtuhumiwa huyo alikuwa akisafiri na ndege ya kampuni ya ndege ya Ethiopia iliyokuwa iondoke jioni ya siku hiyo.

Alisema mtuhumiwa huyo alipokamatwa alipotakiwa kutoa kibali cha kusafirisha mzigo huo hakuwa nacho na alipoulizwa ameyapata wapi alidai ameyanunua kwa wananchi.


Alitaja namba za hati ya kusafiria ya mtuhumiwa huyo kuwa ni 00609687.Alisema upelelezi wa tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na kubaini thamani ya madini hayo.

VIA Nipashe

Monday, December 16, 2013

PICHA YA MANDELA AKIWA KWENYE JENEZA YAWA DILI


 HATIMAYE historia imeandikwa, Mzee Nelson Mandela, rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini amezikwa jana katika shughuli kubwa iliyoshuhudiwa na mamilioni ya watu duniani kote kupitia runinga huku picha ya mwili wake ukiwa ndani ya jeneza ikiwa ndiyo dili kubwa.




Mazishi ya Mzee Madiba aliyefariki dunia Desemba 5, 2013 yalifanyika katika kijiji alichokulia, Qunu, Mkoa wa Mthatha katika Jimbo la Eastern Cape nchini humo.

Wiki iliyopita, serikali ya Afrika Kusini ilitoa amri kwamba haruhusiwi mtu yeyote kupiga picha ya mwili wa marehemu akiwa anaagwa jijini Pretoria.


Familia nayo ikapigilia msumari wa mwisho ikisisitiza kuwa, binadamu yeyote mwenye akili timamu haruhusiwi kupiga picha ya mwili huo ukiwa ndani ya jeneza.
Amri hiyo ilivivunja nguvu vyombo mbalimbali vya habari duniani ambavyo vilikuwa nchini humo vikifuatilia mazishi na maziko ya Mandela.

Serikali iliweka wazi kwamba, mtu yeyote atakayepiga picha, akinaswa zitafutwa kwanza halafu kama ni Msauzi atashitakiwa na kama ni raia wa nje atarudishwa nchini mwake na kupigwa marufuku kuingia nchini humo maishani mwake.

Baadhi ya watu nchini humo wamekuwa wakihaha kupata picha hiyo ili waitengenezee fremu na kuiingiza sokoni kwa wanunuzi.

Juzi, baadhi ya mitandao iliweka sehemu ya sura ya Mandela na kudai ni picha yake akiwa kwenye jeneza siku chache baada ya kifo.

Hata hivyo, haraka sana, baadhi ya vyombo vya usalama nchini humo vilikanusha na kusema picha hiyo ni enzi za uhai wake akiwa amelala.

Ukawekwa ushahidi wa picha hiyo ikiwa yote ambapo Mzee Madiba alikuwa akiuchapa usingizi wakati fulani enzi za uhai wake.

Kuhusu maziko yake, zaidi ya wageni 4,500 kutoka pande zote za dunia walihudhuria ndani ya hema kubwa lililojengwa katika eneo la familia ya Mandela huku mamia ya wanakijiji na baadhi ya wanafamilia  wakikosa nafasi ya kuuaga mwili wa mpendwa wao huyo.


Idadi kubwa ya viongozi waliohudhuria, wakiwemo Rais Barak Obama wa Marekani na mtoto mkubwa wa Malkia wa Uingereza, Prince Charles, kumelifanya eneo la kijiji hicho kuwa dogo na linalohitaji uangalizi wa hali ya juu wa usalama. Katika kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa kiusalama, ndege mbili za jeshi la nchi hiyo zilikuwa angani pamoja na helikopta kadhaa.

Zaidi ya wanajeshi 20,000 walilinda usalama katika kijiji hicho wakifanya kazi sambamba na jeshi la polisi. 

Licha ya wenyeji na majirani hao wa marehemu Mandela kunyimwa fursa ya kuuaga mwili huo, pia walizuiwa kuukaribia kutokana na uhaba wa nafasi, kitendo ambacho kililalamikiwa sana.


Waliokosa nafasi ya kuhudhuria mazishi hayo siyo tu majirani, bali hata mtoto wa kaka mkubwa wa Mandela, Maurice aitwaye Mzwandile Mandela mwenye umri wa miaka 13.

Mwingine ni mpwa wa Mandela, Gloria Mkwedini, mtoto wa dada yake ambaye pia hakuhudhuria mazishi hayo pamoja na familia yake ya watu 16.
Watu hao wanaishi maili chache kutoka kwa Madiba wakiwa wanaishi katika moja ya nyumba nyingi za mduara zilizoko katika eneo hilo.


Na kwa vile hakuna umeme, hawakuweza kufuatilia tukio hilo katika televisheni.
‘Hii imetufanya tujione kama ni watu wageni tuliotengwa,” alisema Gloria akimlaumu mtoto mkubwa wa kike wa Mandela,
 Makaziwe, 59, aliyedai kuwa ndiye aliyekuwa anaamua nani aalikwe na nani aachwe.

Alisema mume wake alimfuata Makaziwe na kutaka kupewa mwaliko, lakini binti huyo alikataa. Alilalamika kuwa kunyimwa kwao mwaliko kunatokana na umasikini wao.

Mandela alizikwa kimila, kwa ndugu wa karibu wa familia yake pamoja na viongozi wa kimila wapatao 70 waliokabidhiwa mwili huo na kuuingiza ndani ya nyumba yake ya milele huku pia wakikataa tukio hilo kurushwa na chombo chochote cha habari.

Miongoni mwa mila na desturi za kabila la Mandela linalofahamika kwa jina la Aba Thembu ni pamoja na kuchinjwa kwa ng’ombe dume aliyenona na damu yake kumwagiwa ndani ya kaburi la marehemu.

Taifa la Afrika Kusini limekuwa lenye pilikapilika nyingi tangu kufariki dunia kwa mpigania haki huyo Desemba 5, mwaka huu, nyumbani kwake jijini Johannesburg baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa mapafu.

Mwili wake uliondolewa saa tisa usiku na kupelekwa katika hospitali ya kijeshi jijini Pretoria ambako kwa siku tatu kuanzia Jumatano, uliwekwa katika majengo ya Ikulu ambako zaidi ya watu laki moja waliripotiwa kuuaga.

Hata hivyo, serikali ilitoa amri ya kusitishwa kwa shughuli hiyo huku maelfu ya wananchi wakiwa katika msururu mrefu wakisubiri kupata nafasi ya kumuaga mtu anayedhaniwa kuwa ndiye maarufu na mwenye heshima zaidi kuliko wote katika karne ya 21


MANGI AAMUA KUTIA KIBERITI NYUMBA YAKE BAADA YA KUBAINI ANASALITIWA NA MKEWE





Baadhi ya Wakazi wa Mtaa wa Ugombolwa, Kata ya Segerea Wilaya ya Ilala Jijini Dar wakishuhudia nyumba hiyo ikiteketea kwa moto.
Segerea, Dar Es Salaam, Nyumba moja iliyopo Mtaa Ugombolwa Kata ya segerea Jijini Dar imeteketea kwa moto mara baada ya baba wa familia ya nyumba hiyo kuhisi kuwa mkewe ana mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine.

Hali hiyo imetokea usiku huu majira ya Saa tano Kasoro usiku katika Mtaa wa Ugombolwa, Kata ya Segerea, Wilaya ya Ilala Jijini Dar Es Salaam ambapo inasemekana baba wa familia hiyo alichukua uamuzi huo mara baada ya kusikia kuwa mkewe ana mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine nje na mara baada ya kutokuelewa kwao ndipo alipochukua uamuzi huo wa kuitia moto nyumba hiyo.
Mmoja wa shuhuda alisikika akisema kuwa "Hawa Wachaga wana matatizo sana Ebu Ona Sasa mwanaume Mzima Anateketeza Nyumba yake aliyoijenga kwa mamilioni ya Shilingi kisa Mkewe anatembea nje ya ndoa Sasa ona watoto wake wataishi wapi?..watu wengine ni wajinga sana Kama mwanamke anatembea nje ya ndoa si umpe talaka tu" alisikika akiongea Shuhuda huyo.

Hakukuwa na dalili zozote zile zilizokuwa zikichukuliwa kwaajili ya kupambana na moto huo huku ikiwa haijafahamika kama wakati nyumba hiyo ikitiwa kiberiti familia ya huyo baba ilikuwepo ndani ya nyumba au laah huku ikikadiriwa kuwa mali zote zilizomo ndani ya nyumba hiyo zimeteketea kwa moto kwani mpaka tunaondoka hakuna kikosi cha zimamoto kilichofik eneo la tukio wala majirani hawakuonyesha dalili zozote zile za kuuzima mot huo.

Mpaka tunaondoka eneo la tukio hakuna taarifa yoyote ile ya majeruhi wala watu kupoteza maisha katika ajali hiyo ya moto.