Pages

Thursday, February 21, 2013

FUNDI UMEME TANESCO ALIENASWA NA UMEME AFARIKI DUNIA



habari tulizozipata hivi punde zinasema kuwa fundi Mbuma amefariki dunia katika hospitali ya mkoa wa  iringa ajali hii ilitokea baada ya wafanyakazi wenzake kuwasha umeme kimakosa alipokuwa akifanya matengenezo juu ya nguzo za umeme


Fundi wa Shirika la Umeme Tanesco mkoani Iringa, Selemani Mbuma akiwa amenaswa na umeme baada ya wenzake kuwasha umeme kimakosa wakati akiendelea na matengenezo katika eneo la Mlandege mkoani humo.






WATUHUMIWA MAUAJI YA PADRI MUSHI WAKAMATWA WAKIJARIBU KUTOROKA


*Wadaiwa kusafiri kwa Jahazi kutoka Z’bar hadi Mombasa
*Wanaswa katika usafiri wa gari wakielekea mjini Nairobi

MAKACHERO wa Jeshi la Polisi nchini wamewatia mbaroni vijana watatu wanaotuhumiwa kuhusika katika mauaji ya Padri Everist Mushi (55) wa Kanisa Katoliki mjini Zanzibar.

Watuhumiwa hao wamekamatwa mjini Nairobi, Kenya kutokana na ushirikiano w...
a Jeshi la Polisi la Tanzania na Polisi wa Kenya kwa mwamvuli wa Shirikisho la Polisi wa Kimataifa (Interpol).

Habari za kuaminika kutoka Nairobi, Kenya zimesema kuwa watuhumiwa hao ambao majina yao yamehifadhiwa, walitiwa nguvuni juzi mjini humo walipowasili wakitokea Mombasa, mashariki mwa nchi hiyo.

Watuhumiwa hao ambao walikuwa wakiingia katika maficho kukwepa mkono wa dola, wanadaiwa kutumia jahazi kusafiria kutoka Zanzibar hadi Mombasa, Kenya kabla ya kusafiri kwa magari hadi Nairobi ambako walitiwa nguvuni.

Habari na Jamii Forums.





R.I.P

Wednesday, January 30, 2013

KESI YA TUHUMA ZA KUBAKA NA KUSABABISHA MIMBA YA MCHUNGAJI MWASUMBI MBEYA YAFUFUKA





Mchungaji wa Kanisa la EAGT la Iwambi Jijini Mbeya Daniel Mwasumbi (57), Jana alipandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya Gilbert Ndeuluwo akituhumiwa  kumbaka na kumpa Mimba mwanafunzi.

Akisoma mashtaka hayo Mwendesha mashtaka wa Serilkali Archiles Mulisa alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo kati ya Mwezi Januari 2008 ambapo alimbaka na kumpa ujauzito Neema Boni (17) ambaye ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari Itende.

Mulisa alidai mahakamani hapo kuwa kosa hilo ni kinyume cha kanuni ya elimu ya 5 ya gazeti la Serikali namba 265 ya mwaka 2003 na chini ya Sheria ya elimu namba 25 ya mwaka 1978 ambapo mshtakiwa anatuhumiwa kutenda makosa mawili ikiwemo kubaka na kusababisha ujauzito.

Aliongeza kuwa kosa la kubaka ni kinyume cha kanuni ya adhabu kifungu cha 130(1),(2)(e) na cha 131(1) kama kilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hata hivyo mshtakiwa huyo alikana mashtaka yote ambapo  aliachiwa kwa dhamana ya Shilingi Milioni Mbili na mdhamini mmoja mwenye barua kutoka taasisi inayotambulika, kesi hiyo iliahirishwa hadi Januari 30 itakapoanza kusikilizwa.

kwa hisani ya Mbeya yetu








Tuesday, January 29, 2013

Na Mercy Mwalusamba
Iringa
Wanawake waendelea kutupa au kutelekeza watoto Nchini
Utupaji wa  watoto hivi sasa umekua kama fasheni kila mahali kumekuwa na kasumba hii ya kutupa watoto mara tu wazaliwapo kana kwamba ni taka ambazo ni kawaida kuzikuta jalalani
Ukatili huo hufanywa mara nyingi na wazazi ambao ama hawana mipango ya kuchukua jukumu la kuwalea watoto hao au kutokana na sababu moja au nyingine, huku wengi wakiokotwa barabarani, kwenye majalala ya taka, vyooni na wengine wakiwa wametelekezwa mahospitalini
Kila binadamu ana haki ya kuishi awe amezaliwa katika hali ya ulemavu wa aina yoyote au awe amezaliwa katika familia duni hivyo  ndivyo Mungu alivyopanga  hivyo yeye kama binadamu ana haki ya kuishi kama binadamu wengine
Wanawake wanaotupa watoto wamekuwa na visingizio lukuki pindi wanapobainika na makosa hayo na kuhojiwa kusingizia maisha magumu au kusingizia kuzaa mtoto mlemavu kukataliwa na wazazi wenzao wanaowapa mimba japo sababu hii inahusiana sana na suala lenyewe lakini si sawa na si haki kutupa kiumbe kilichoumbwa kwa makusudi ya Mungu
Suala la kutupa watoto kila mtu linamuhusu awe mwanamke ambae ndie muhusika mkuu lakini pia linamuhusu mwanaume kwasababu mtoto hutengenezwa na watu hawa wawili hivyo ushirikiano katika hili  unapaswa kuwepo kuanzia kipindi cha ujauzito hadi mtoto anapozaliwa
Japo suala la kukataa kwa mwanaume kua sie muhusika wa mimba ndio limekua limechukua nafasi kubwa lakini sitaki  kuamini kwamba ndio sababu kuu ya kumpelekea mwanamke kutupa mtoto
 Mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu mwenyewe huna haki kisheria huna haki ki imani wala hakuna utamaduni wa kutupa mtoto kwa kabila lolote unapaswa ujue kwamba Mungu anakushangaa na bina damu wanakushangaa kwa ukatili huo
Wanawake wanaosingizia ugumu wa maisha kwamba maisha yake magumu hana uwezo wa  kulea mtoto  uamuzi wa mwisho unaoufikia wakuamua  kwenda  kutupa mtoto  jalalani bado hutendi haki wewe una dhambi tu tena kubwa sana
Kuna baadhi ya wanawake  wanazeeka hajawahi kubeba hata ujauzito ni stori kwake anatamani hata Mungu amjaalie  kupata mtoto taahila  ili mradi tu asionekane mgumba  wengine wamekula hata vinyesi lakini ameshindwa mwingine  lakini wewe unabeba Rambo iliyowekwa mtoto kama taka taka unaenda kutupa jalalani huna tofauti na muuaji
Serikali iangalie adhabu nyingine katika hili ikiwezekana adhabu ibadilishwe na iwe kali zaidi  adhabu iliyopo haiogopwi hata kidogo
kuna njia nyingi za uzazi wa mpango na asilimia kubwa ya wanawake wana elimu hii ya uzazi wa mpango kwanini wasichukue hatua ya kuzitumia ukizingatia hazina gharama yoyote  kuzipata serikali imetoa bure
Ingekua ni vyema kuzuia mapema kama haupo tayari kwa wakati huo kupata mtoto lakini cha ajabu unalea mimba kwa miezi tisa au chini ya hapo ambapo tayari Mungu kafanya uumbaji wake mtoto anazaliwa unatupa
mapema wiki hii mtoto amekutwa ametupwa maeneo ya M.R amekutwa akiwa amekufa ndani ya mfuko wa kusafiria  kabla ya tukio hilo mtoto mwingine aliokotwa karibu na Chuo cha Tumaini University mkoani Iringa  wanawake wanaosifika kwa huruma na kuwa walezi wazuri wa familia wenye mapenzi amebadilika na kua kama mnyama
wengine wamekua wakizaa watoto wazima na kuwanyonga kisha kuwatupa hata hofu ya Mungu haipo kabisa kwao hakuna imani ya dini yoyote inayoruhusu ukatili wa namna hii labda dini ya mashetani
Na hili limekua ni chanzo cha watoto wa mitaani kwasababu baadhi yao akija kugundua ukweli wa maisha yake anashindwa kujikubali  na kuadhirika kisaikolojia na huishia mitaani
imefika wakati sasa wanawake watambue umuhimu na haki ya mtoto ya kuishi kwani wanawake wamekuwa wakibeba ujauzito na kisha kutoa mimba huku wanawake wengine wakitupa watoto wachanga pindi wanapojifungua

Wanawake waepukane na mimba zisizotarajiwa hii itasaidia kupunguza tatizo la watoto wachanga kutupwa au kunyongwa pindi wazaliwapo
Ikishindikana wafuate uzazi wa mpango hospitali inatoa huduma bure na siyo kutupa mtoto ambaye umemlea kwa miezi 9 tumboni leo hii mama anajifungua na kutupa mtoto huo ni ukatili wa hali ya juu kwa mtoto asiye na hata chembe ya hatia
..........................................MWISHO...............................................................

MTOTO ALBINO AKIWA AMETUPWA JALALANI ARUSHA

KICHANGA KILICHOTUPWA PEMBENI MWA MTO KARIBU NA CHUO KIKUU TUMAINI IRINGA


 


Monday, January 28, 2013

HATIMAYE MAHAKAMA IMETANGAZA DHAMANI KWA MWIGIZAJI LULU MICHAEL PAMOJA NA MASHARTI ANAYOTAKIWA KUYAFUATA

Mahakama kuu leo imetangaza dhamana ya mwigizaji Lulu lakini iwapo atatimiza masharti aliyopangiwa ambayo ni pamoja na kuwasilisha hati yake ya kusafiria,

 kutosafiri nje ya Dar es salaam, kujiwakilisha au kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila mwezi pamoja na wadhamini wake wawili ambao kila mmoja adhamini kwa shilingi milioni 20 za kitanzania.

Upande wa familia ya Lulu umesema masharti yote yaliyotajwa wanaweza kuyatimiza leo leo hivyo wanasubiri tu jibu la msajili ambae ndio anatakiwa kuhakikisha hayo masharti yametimia kisha ruhusa ya kumkabidhi Lulu kwa familia yake itolewe.

Taarifa za ndani ni kwamba uwezekano wa Lulu kuachiwa upo kuanzia january 29 2013 ambayo ni kesho kwa sababu kuna watumishi wawili wa serikali ambao wapo kikazi mkoani Pwani na ndio walitakiwa kutia saini dhamana ya Lulu wakiwa ni sehemu ya masharti.


 Lulu akiwa mahakamani leo


aleshika maji ni mama yake Lulu

Thursday, January 3, 2013

MANENO YA MWISHO YA SAJUKI





Mwigizaji Dinno alikua rafiki mkubwa sana wa Marehemu Sajuki na ndio alikua analala hospitali na Sajuki pale Muhimbili.

Ameongea Exclusive na AMPLIFAYA ya CLOUDS FM na kutoa maneno ya mwisho ambayo aliyasikia kutoka kwa Sajuki akimzungumzia mke wake ambae ni Wastara.

Kwa haraka haraka mwigizaji Wastara amesifiwa sana na watu mbalimbali kwa moyo wake wa ushujaa wa ukweli wa upendo kwa Sajuki japo walipitia matatizo makubwa na mengi kwenye maisha yao.

Masanja Mkandamizaji na Arnold Kayanda ni miongoni mwa mastaa wa Tanzania waliopaza sauti zao kupitia mitandao ya kijamii kumsifia Wastara kwa moyo wa upendo.

Tukirudi kwa Dinno, namkariri akisema “tulipokuwa Arusha sisi watatu tu Sajuki alionyesha ishara ya kukata tamaa, siku moja tulikua hotelini usiku kama saa tisa hivi Wastara alikuja kuniamsha kwenye chumba changu nikaenda kwa Sajuki, alikua anaumwa sana akamwambia Wastara naomba mpigie mama niongee nae, Sajuki akamwambia mama yake mzazi kwamba Wastara nampenda sana, kanizalia mtoto mzuri anaitwa Farhini, naomba msimsumbue naomba msimpe shida yoyote amenisaidia sana, naomba mumwachie Farhini amlee amtunze mtamuona, yalikua maneno mazito sana mpaka machozi yakawa yananitoka”

Kwenye mstari mwingine Dinno amesema jambo jingine ambalo Sajuki aliliongea mwishoni ni kuhusu upendo miongoni mwa wasanii wa movie Tanzania, namkariri akisema “alikua ananiambia hebu jitahidi kuwa unakaa na wasanii, unajua sisi hatupendani Dinno ila mimi iko siku nitakuja kuropoka nikae na watu niwazungumzie tuweke upendo pamoja, tukishapendana tutafanya kitu Dinno”

Wednesday, December 26, 2012

PADRI APIGWA RISASI ZANZIBAR


Zanzibar, padri Ambrose Mkenda amepigwa risasi na watu wasiofahamika wakati akifunguliwa geti aingie nyumbani kwake maeneo ya Kitomondo mjini Zanzibar.

Waliompiga risasi walikuwa kwenye pikipiki na wametokomea kusikojulikana!!!!!!!