Pages

Friday, May 24, 2013

MWANDISHI NGULI WA NIGERIA CHINUA ACHEBE AZIKWA

 CHINUA ACHEBE ENZI ZA UHAI WAKE


 BAADHI YA WAOMBOLEZAJI WAKIWA WAMEBEBA JENEZA 


BAADHI YA WASHIRIKI KATIKA MAZISHI YA MWANAFASIHI NGULI MAREHEMU CHINUA ACHEBE WAKIWA WAMEVALIA MAVAZI YA KIMILA YA NIGERIA YALIYOFANYIKA JANA KATIKA JIMBO LA ANAMBRA

Melfu ya waombolezaji walijitokeza kwa mazishi ya mwandishi mashuhuri wa nchi hiyo marehemu Chinua Achebe, katika jimbo la Anambra.Wageni mashuhuri akiwemi, rais Goodluck Jonathan pia hawakuachwa nyuma.

Mamia ya watu walikusanyika kanisani baadhi wakivalia mavazi ya kitamaduni yenye picha ya Achebe. Marehemu Achebe alisifika sana kama baba mwanzilishi wa fasihi ya kiingereza barani Afrika.

kwa  hisani ya BBC

Thursday, May 23, 2013

HALI ILIVYOKUA LEO MTWARA











 BAADHI ya wananchi wa eneo la magomeni mkoani Mtwara wamekimbilia katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara Lugula wakihofia usalama wao kutokana na vurugu za kuchomwa kwa nyumba zao pamoja na vibanda vya biashara zilizotokea leo asubuhi katika eneo hilo

Kwa sasa inaelezwa kuwa katika baadhi ya mitaa hali imetulia na ni idadi ndogo ya wananchi ndiyo inayoonekana wakitembea mitaani isipokua eneo la magomeni ambako mbomu yanaendelea kusikika huku huduma za kijamii katika mji huo zikiwa zimesimama zikiwemo usafiri, huduma za kibenki na shule

RAISI AZINDUA BARABARA YA IRINGA DODOMA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI KATA YA MIGOLI

Na







 Iringa
RAISI wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya  Mrisho Kikwete  jana amefanya uzinduzi wa barabara mpya ya Iringa Dodoma yenye urefu wa kilomita 260 na kuweka jiwe la msingi katika  ya kata ya Migori jimbo la Isimani Mkoani Iringa
Alisema kutokana na kuwa na mahusiano mazuri na wafadhili kutoka nchi za nje ujenzi wa barabara hiyo umewezeshwa na  mikopo kutoka benki ya serikali ya Japan na benki ya maendeleo ya Afrika   pamoja na serikali  ya Tanzania.
Kikwete alisema lengo la serikali ni kuunganisha barabara zote zinazounganisha mikoa zenye kiwango cha chini kua na kiwango cha lami na kwamba  barabara hiyo ni moja ya barabara kuu za Afrika  hivyo kuwepo kwa  barabara hiyo kutainua utalii na kukuza  uchumi  wa mkoa na nchi kwa ujumla
‘’bila shaka serikali imejitahidi kujenga barabara na lengo la serikali ni kuunganisha barabara zote  japokua ujenzi wake ni ghali sana lakini pia kuna manufaa makubwa  na barabara hii tunatarajia kuimaliza mwaka 2015’’
Alisema barabara ya Iringa Dodoma itawasaidia wananchi wa kusini kwenda mikoa ya kaskazini  kwa urahisi ukitofautisha na usumbufu ulikuwepo awali ambapo wananchi walilazimika kipita Chalinze  kwenda mikoa ya Arusha
Pia raisi Kikwete alieleza kuwa barabara  ya Iringa Dodoma itagharimu kiasi cha Tsh Bilioni 232.2 na kwamba kiasi cha shilingi Bilioni 1.9 kilitumika kuwalipa fidia baadhi ya wananchi waliokuwa na makazi ndani ya hifadhi ya barabara hiyo.
Hata  hivyo Jakaya amewaasa wananchi wanaoizunguka barabara hiyo kuacha kurudisha nyuma shughuri za maendeleo kwa kuiba baadhi vitendea kazi vikiwemo vipuli pamoja na mafuta kwani kwa kufanya hivyo wanarudisha nyuma maendeleo yao wenyewe.
Mbali na hayo raisi Kikwete amewaasa wananchi kuwa makini na gonjwa hatari la Ukimwi kwani uwepo wa barabara hiyo utaongeza idadi kubwa ya watu hivyo kuchukua tahadhari mapema.
‘’Uwepo wa barabara hii utaongeza wingi wa watu na wingi wa magari hivyo nawaasa kua makini kwa kupalamia wageni hovyo kwasababu barabara hii itatumika na watu tofauti kutoka nchi mbali mbali’’Alisema
Nae waziri wa ujenzi Dk John Magufuli alisema wakandalasi watakaozembea katika shughuri nzima ya kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo serikali haitawavumilia na badala yake watafukuzwa
Magufuli  amempongeza Mbunge Wa Isimani William Lukuvi kwa uchapa kazi wake na kwamba endapo mbuge huyo angeamua kugombea jimboni kwake basi asingeweza kusimama nae bali angemuachia.

Thursday, May 16, 2013




 Sister Feki Phylis Wanjiru Kamau.

 JESHI la polisi mkoa wa Iringa limemkamata mwanamke Phylis Wanjiru mwenye umri wa miaka 44 aliyevalia mavazi ya kitawa wa masister wa kanisa Kathoriki, ambapo baada ya kupekuliwa amekutwa na baadhi ya vielelezo vilivyobaini kuwa ni tapeli.

Wanjiru ambaye ni raia wa nchi ya Kenya amekamatwa na jeshi la polisi baada ya masister wenzie kubaini kama si mmoja wao, kutokana na kushindwa kufanya baadhi ya masuala  ambayo ni msingi wa utawa wao.

Akizungumzia mkasa huo, kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda amesema mwanamke huyo kabila laKe ni Muwembu wa nchini Kenya amekamatwa katika nyumba  za masista zilizopo Ipogolo mjini Iringa.

Aidha Kamuhanda amesema mwanamke huyo ambaye awali aligoma kutoa maelezo ya kina juu ya ujio wake nchini Tanzania, katika upekuzi walimkuta na baadhi ya chip (Line) za makampuni mbalimbali ya simu ya ndani na nje ya nchi.

Kamuhanda amesema Sister huyo bandia alikutwa pia akiwa na hati za kusafiria (Passport) mbili, moja ikiwa niya Africa Mashariki yenye namba Ke. 020659 huku hati ya nyingine ikiwa na jumuiya ya Kenya namba A. 1790366.

Amesema Sister huyo feki katika hati hizo ilionyesha kuwa alitembelea nchi ya Rwanda, Uganda pamoja na nchini Tanzania ambapo siku za hivi karibuni alikuwa Mkoani Mara Tarime.

Sister huyo FEKI amekuwa akitumia mbinu ya kujiangusha kama mtu mwenye ugonjwa wa kifafa pindi anapofanyiwa mahojiano, jambo linalowawia vigumu jeshi hilo kupata maelezo ya kina dhidi ya dhamira yake ya kuingia humu nchini.

Kamuhanda ameitaka jamii kuwa makini na wageni mbalimbali, huku akiwaasa kuacha tabia ya kuwaamini watu kwa muonekano wao, kutokana na mwanamke huyo kutumia njia hiyo ambayo inamfanya kila mtu kumuamini.

Wema: “Ni kweli picha ni romantic lakini yule kijana (Raheem) si mpenzi wangu. Naomba nieleweke hivyo.”





WEMA ambaye ni Miss Tanzania mwaka 2006, huku akifurukuta kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, ametokelezea na mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina moja la Raheem katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

GUMZO MITANDAONI
Picha hiyo ambayo pozi lake ni ‘very romantic’ imezua gumzo katika mitandao mbalimbali ilipotundikwa na wadau wengi walionekana kuamini kuwa Wema alikuwa akimnadi mpenzi wake mpya.
Mtoa maoni mmoja aliandika: “Naona Wema ameamua kutuonesha shem wetu mpya, sasa hapo kazi kwa wenye vijicho.”

Mwingine aliandika: “Mmh! Mbona (Raheem) haonekani uso? Kama lengo lake lilikuwa kumwanika angemuacha tu aonekane ila dah! Ana kifua kizuri sana. Huyu jamaa anaonekana anafanya sana mazoezi.”
DIAMOND ATAJWA

Katika gumzo hilo, wengine walikwenda mbali zaidi, wakisema kwamba inawezekana Wema alikuwa na Raheem kwa siri muda mrefu lakini sasa ameamua kuvunja ukimya ili kumringishia x – boyfriend wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
INTERVIEW NA RAHEEM
Ni jadi ya magazeti ya Global Publishers likiwemo hili la Risasi Mchanganyiko kutafuta mzani wa habari kabla ya kwenda hewani hivyo lilimtafuta Raheem ambaye alitoa ushirikiano wa kutosha.
Raheem alikiri kuitambua picha yake na Wema lakini alisema imemshtua na kumcha-nganya maana hakutegemea kama ingefika mitandaoni na hatimaye kwenye vyombo vya habari.

Alisema: “Ni kweli nilipiga hiyo picha na Wema lakini ni ya kawaida tu, haina maana nyingine tofauti. Wema ni rafiki yangu na dada yangu. Tunaheshimiana, hakuna cha zaidi.

“Wema ni maarufu na watu wanaweza kujaji wanavyotaka, hilo litanisababishia matatizo kwa sababu mimi nina mpenzi wangu na Wema si mtu wangu kabisa…she is just my sister (ni dada yangu tu).”
Risasi: Hiyo picha mlipiga lini, wapi na kwa matumizi gani?Raheem: Ilikuwa kwenye function (tukio) fulani ambayo siwezi kuizungumzia. Kama wiki sita au miezi miwili hivi iliyopita na tulipiga kama marafiki tu, hakuna cha zaidi.
Risasi: Kwa hiyo Wema akithibitisha wewe ni mpenzi wake itakuwaje?Raheem: Nitamshangaa sana! Wema ni dada yangu tu.Risasi: Inasemekana Wema ameamua kuianika hiyo picha kwa lengo la kumrusha roho Diamond, unasemaje hapo?

Raheem: Sijui na kwa kweli siwezi kuzungumzia mambo ya mtu binafsi. Sijui chochote.
Wema alipatikana na kusomewa mashitaka yake ambapo alikiri kupiga picha na Raheem, akafafanua kuwa aliipiga muda mfupi baada ya kutoka kufanya interview na kituo kimoja cha redio (jina kapuni) lakini akasema haina uhusiano wowote na suala la mapenzi.
“Ni kweli nilipiga hiyo picha, yeye aliniomba tu kama fan (shabiki) wangu, akataka ku-show love (kuonesha upendo), sikuona sababu ya kumkatalia. Nakumbuka siku hiyo nilikuwa na Martin (Kadinda – meneja wake) na baada ya siku hiyo sijawahi kuonana naye tena mahali popote…sioni tatizo kabisa, ni kawaida kwa sisi mastaa,” alisema Wema.
Risasi: Lakini Wema wadau wanasema eti ni mpenzi wako na umefanya hivyo kwa lengo la kumrusha roho Diamond.
Wema: Umeshasema wadau, waache na mambo yao lakini maelezo yangu ni hayo na naamini yamejitosheleza.
Risasi: Kuna kitu nahitaji ufafanue zaidi…lile pozi lipo romantic sana, hufikiri kuwa inaweza kuwa sababu ya watu kuwa na hisia kwamba ni mpenzi wako?
Wema: Ni kweli picha ni romantic lakini yule kijana (Raheem) si mpenzi wangu. Naomba nieleweke hivyo. Ahsante

Tuesday, May 14, 2013

MASKINI ANGELINA JOLIE AKATWA MATITI YAKE NA KUONDOA MFUKO WAKE WA UZAZI







 MCHEZAJI wa filamu mashuhuri sana duniani,Angelina Jolie amesema kwamba amekatwa matiti yake yote pamoja na kuondoa mfuko wake wa uzazi.

Kwenye taarifa aliyoandika kwenye gazeti la New York Times, Bi Jolie amesema alifanyiwa uchunguzi wa celi zake na kugunduliwa kwamba alikuwa katika hatari kubwa sana ya kupata saratani ya matiti. Ndipo akaamua kukatwa matiti yake mawili.

Angelina mwenye umri wa miaka 37 na mama na watoto sita, alipoteza mamake mzazi kutokana na maradhi ya saratani ya matiti.

Anasema aliandika taarifa hiyo kuwahakikishia watoto wake kwamba hakuwa kwenye hatari ya kupata saratani tena.

Kulingana na Jolie madaktari walisema kuwa uwezekano wake kupata Saratani ya matiti ni asilimia 87 huku akiwa na asilimia 50 uwezo wake wa kuugua Sarati ya mfuko wa uzazi.

''Niliamua kuchukua hatua mwenyewe ili kuzuia uwezekano wowote wa kuugua Saratani hiyo,'' alisema Jolie.

Alisema kuwa shughuli hii ilianza mwezi Februari na kukamilika mwishoni mwa mwezi April.
Katika taarifa iliyoandikwa na Bi Jolie na yenye kichwa, 'Uamuzi wangu wa kimatibabu', Bi Jolie alieleza kuwa mamake alipambana na Saratani kwa miaka kumi na kufariki akiwa na umri wa miaka 56.


Alisema kuwa alielewa fika kuwa siku moja atawahi kuugua Saratani na ndio maana akachukua uamuzi wa kufanyiwa upasuaji huo mgumu wa wiki tisa ambao ulihitaji kukatwa matiti.

Uwezekano wake wa kuugua saratani sasa umeshuka kutoka 87% hadi 5%.
Alimsifu mumewe Brad Pitt, kwa kumuunga mkono na kumfariji kwa kila aliyopitia, na kusema kuwa ametulizwa na kuwa wanawe hawakupata lolote katika matokeo ya uchunguzi wa madaktari tangu kufanyiwa upasuaji.


"ninahisi kuwa na nguvu kwa uamuzi niliofanya, na kwa kuwa ninasalia kuwa mwanamke hata baada ya kuondoa viungo hivyo,'' alisema Bi Jolie.

"kwa mwanamke yeyote anayesoma maneno haya, natumai ataweza kujua kuwa wanaweza kufanya uamuzi.''

Muigizaji huyo, ambaye ameshinda tuzo nyingi kwa uigizaji wake, pia ni mtunzi wa filamu na mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa anayehusika na harakati za kibinadamu.

Wakati alipokuwa anafanyiwa upasuaji, Bi Jolie alizuru Jamuhuri ya Kidremokrasia ya Congo pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague.

Friday, May 10, 2013

WAENDESHA DALADALA WAGOMA KUSAFIRISHA ABIRIA LEO MJINI IRINGA



 mmoja wa madereva wa daladala akiwatuliza madeveva wenzie
Ofisa  wa  Sumatra  mkoa  wa Iringa Rahim Kondo





usafiri uliotumika leo kubeba abiria

Mgomo  wa  daladala katika Manispaa ya Iringa umeanza asubuhi hii katika eneo la Mwang'ingo mjini Iringa kwa  madereva na   wamiliki   wa  daladala mjini hapa kudai  kuchoshwa na manyanyaso ya afisa mpya  wa SUMATRA mkoa  wa  Iringa.
Habari  ambazo  mtandao huu umezipata zinadai  kuwa hatua ya  mgomo huo  imekuja   kutokana na kuchukizwa  uamuzi  wa Sumatra  mkoa  wa Iringa  kufuta  stendi ya  posta pamoja na  kuzuia daladala  kukaa kwa muda  eneo la stendi ya  daladala  ya Miyomboni maeneo ambayo  kimsingi  walikuwa  wakikaa siku zote. 
Madereva  hao  wamesema  kuwa leo  hawapo   tayari  kufanya kazi hadi  hapo afisa  huyo  wa Sumatra  mkoa  wa Iringa atakapofuta maagizo yake ya  kuzuia stendi hiyo ya  posta na kuruhusu daladala  kukaa muda zaidi  eneo la Miyomboni.

Hali  hiyo  imeanza  kutikisha  na kufanya  polisi  kuingilia kati  kuwatuliza  madereva  wasigome jitihada  zinazoendelea  hadi  sasa.

Hata  hivyo usafiri  unaofanya kazi ni bajaji  ,pikipiki na Taxi ambapo nauli  kwa kichwa katika bajaji  Tsh. 3000 wakati Taxi kwa kila kichwa Tsh 1000