Thursday, February 20, 2014
WATOTO WALIO ZALIWA WAMEUNGANA WAREJEA NCHINI BAADA YA KUTENGENISHWA
Watoto pacha, Elikana na Eliud waliokuwa wameungana wamerejea nchini jana wakitokea India walipokuwa kwa ajili ya kutenganishwa, tayari kwa kusherehekea kumbukumbu yao ya kutimiza mwaka mmoja leo.
Waliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere saa 10:30 kwa ndege ya Shirika la Ndege la Oman, wakiwa na mama yao, Grace Joel (20) ambaye muda wote alionekana mwenye furaha.
Elikana na Eliud walizaliwa Februari 20, mwaka jana wilayani Kyela, Mbeya wakiwa wameungana na baadaye kuhamishiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambako walipata rufaa ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Juni mwaka jana, Serikali iliwapeleka Hospitali ya Chennai, India ambako Desemba 16, mwaka jana walifanyiwa upasuaji mkubwa wa kuwatenganisha.
Akizungumza baada ya kutua jana, Grace alisema: “Nina furaha ya ajabu, sijui nimshukuru vipi huyu Mungu wangu, ni mkuu mno. Ninawashukuru sana madaktari wa India, ninawashukuru madaktari wa Muhimbili na sana naishukuru Serikali yangu kwa kunipa msaada huu mkubwa. Siamini kama leo ningekuwa narudi salama na watoto wangu kila mmoja akijitegemea,” alisema Grace.
“Kesho (leo) ni birthday yao, wanatimiza mwaka mmoja, ni furaha ya ajabu niliyo nayo, siwezi kuelezea. Siku nilipoambiwa watoto wangu watafanyiwa upasuaji mkubwa na watapumulia mashine kwa wiki moja, nilichanganyikiwa kwa kweli, sikutamani tena hata hiyo operesheni ifanyike ila sikuwa na jinsi zaidi ya kumwomba Mungu.”
Akizungumza uwanjani hapo, Dk Glory Joseph kutoka Hospitali ya Rufaa Bugando ambaye aliongozana na watoto hao kurudi nchini alisema: “Watoto wamerejea salama na wanaendelea vizuri ila watakuwa Moi (Hospitali ya Mifupa Muhimbili), kwa uangalizi maalumu mpaka hapo madaktari watakapoona inafaa ndipo watapewa ruhusu ya kurudi nyumbani kwao Mbeya.
“Agosti watarudishwa tena India kwa ajili ya upasuaji katika njia ya mkojo na kufunga sehemu ya utumbo,” alisema.
Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamwaja alisema upasuaji wa watoto hao ulichukua saa 18. Katika muda huo, saa 13 zilitumika kutenganisha viungo vilivyoungana sehemu ya chini ya uti wa mgongo, sehemu ya utumbo mpana, njia ya mkojo, kibofu na sehemu ya uume, wakati saa tano zilitumika kuunganisha sehemu zilizotenganishwa.
Pacha hao walifanyiwa upasuaji na madaktari 20 na wataalamu wengine wa afya ambao walitumia saa 18 kuwatenganisha. Kiasi cha Sh100 milioni kilitumika.
Meneja wa Huduma za Wagonjwa wa Kimataifa wa hospitali hiyo, Senu Sam alizungumza na gazeti dada la Mwananchi, The Citizen juzi na kusema wamefanya sherehe kwa ajili ya mafanikio ya upasuaji huo.
Sam alisema pacha hao wameonana ana kwa ana kwa mara ya kwanza, wiki tatu baada ya upasuaji... “Imekuwa faraja kuwaona wakitazamana. Eliudi alivishika vidole vya mkono wa Elikana na kuvichezea. Wanaonekana kufurahia
Thursday, February 13, 2014
KESI YA DAUDI MWANGOSI YAANZA KUSIKILIZWA
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa, Frank Leonard
( wa nne kushoto mwenye begi ndogo begani) akiwa nje ya mahakama kuu
kanda ya Iringa na wanahabari wengine mara baada ya kesi ya mtuhumiwa wa
mauaji ya Daudi Mwangnosi kusikilizwa
Waandishi wakisubiri kupiga picha ya mtuhumiwa bila mafanikio hadi wanaondoka eneo la tukio (mahakamani)
KESI
ya mauaji ya aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Channel Ten Mkoani Iringa, Daudi
Mwangosi imeanza kusikilizwa hii leo baada ya kilichoelezwa na upande wa mashtaka
kwamba uchunguzi wake umakamilika.
Kama
ilivyo ada, makechero wa Polisi wengi wao wakiwa wamavaa kiraia walikuwepo
mahakamani hapa huku wakijaribu kuwazuia wanahabari kutekeleza wajibu wao.
Katika
mazingira ya kutatanisha, mwandishi wa habari wa gazeti la Habarileo, Frank
Leonard ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa
alikamatwa na askari wanne waliokuwa wamevaa kiraia kwa kile kilichoelezwa
kwamba alikuwa akipiga picha mahakamani wakati kesi ikiendele
Baada
ya kukamatwa Leonard, alifikishwa kituo cha Polisi cha Kati mjini Iringa na
kuachiwa huru baada ya kukosekana ushahidi.
Akizungumza na wanahabari baada ya kuachiwa huru, Leonard alisema "wapo
baadhi ya askari kwa makusudi wanataka kubomoa mahusiano baina ya wanahabari na
jeshi la Polisi ambayo yanaendelea kujengwa na kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Iringa, Ramadhani Mungi."
Alisema
kitendo cha kubambikiziwa tuhuma ndani ya muhimili wa dola unaojitegemea
(mahakama) ni kitendo cha uzalilishaji kinachotaka kuaminisha umma kwamba
wanahabari ni watu wasiotaka kufuata taratibu za kimahakama.
Alisema akiwa ndani ya chumba cha mahakama hiyo alikamatwa na askari hao bila
idhini ya Jaji wa Mahakama Kuu wakati akizima simu yake ya mkononi iliyokuwa
katika mtetemo.
"Nilikuwa nazima simu yangu hao askari hao kwasababu wanazojua wao wenyewe
waligeuza suala hilo ili lionekane katika sura wanayoitaka na hatimaye
wanifungulie mashtaka," alisema.
Alimshukuru
Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Iringa, Ngoi kwa kumtendea haki na baada ya
kupata ushahidi kufutilia mbali kesi hiyo.
Akizungumza na wanahabari, Msajili wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Dunstan Nduguru aliwashangaa Polisi kwa kuingia shughuli za mahakama.
"Hata
kama mwandishi huyo angekuwa anapiga picha, haikuwa kazi yao kumkamata mpaka
wapewe agizo na Jaji Mfawidhi aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo," alisema.
Pamoja
na askari hao kuwazuia wanahabari kuchukua picha mara baada ya mtuhumiwa huyo
kufikishwa mahakamani, Nduguru alisema utaratibu wa mahakama unawaruhusu
wanahabari kuchukua picha kabla shughuli kabla shughuli za mahakama hazijaanza
na baada ya shughuli hizo kwisha.
"Kuwazuia
wanahabari kufanya kazi zao kwa utaratibu huo sio sahihi; siku nyingine mkiona
kuna dalili ya kupata bugudha kama hiyo naomba mnijulishe ili niondoe mzozo
huo," alisema.
Mbele
ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Mary Shangali,
Wakili wa upande wa mashtka, Adolph Maganga alisema Adolph Maganda alisema kwa
kukusudia mtuhumiwa Pacificius Cleophace Simoni anatuhumiwa kumuua Mwangosi
kinyume na kifungu cha sheria ya kanuni ya adhabu namba 196 sura ya 16
kilichofanyiwa marejeo mwaka 2002.
Alisema katika tukio hilo lililotokea Septemba 2, 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa, mshtakiwa alifyatua bunduki yake na kusababisha kifo cha marehemu, papo hapo.
Alisema
siku ya tukio marehemu alikuwa Nyororo kwa ajili ya kuripoti na kutoa taarifa
kwa umma juu ya mkutano uliokuwa ufanywe na katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema).
Alisema mshtakiwa akiwa mmoja wa wafanyakazi wa Polisi, waliwasihi Chadema wasifanye mkutano huo kabla wafuasi wake hawajaanza kurusha mawe kwa Polisi na baadhi yao kupata majeraha.
Kutokana
na mzozo huo, wakili huyo wa serikali alisema polisi walipiga mabomu ya machozi
ili kuwatawanya wafuasi hao kabla mshtakiwa huyo hajamfyatulia bomu marehemu.
Wakili
huyo aliwasilisha ramani ya eneo la tukio, ripoti ya mtaalamu wa milipuko na
ripoti ya daktari aliyechunguza mwili wa marehemu Mwangosi na gazeti la Mwananchi
la Septemba 3, 2012 lililochapisha picha ya tukio hilo katika
ukurasa wa mbele kama vielelezo vinavyohusiana na kesi hiyo.
Wakili
wa upande wa utetezi Lwezaula Kaijage alitaja mambo wanayokubaliana katika kesi
hiyo kuwa ni jina na anuani ya mshtakiwa na kwamba marehemu Mwangosi alikufa
kifo ambacho si cha kawaida.
Na
kwamba mshtakiwa Simoni alikamatwa na amefikishwa mahakamani akihusishwa na
mauaji hayo.
Wakili
Kaijage alisema vielelezo vingine vilivyoletwa na upande wa mashtaka
hawakubaliani navyo kwakuwa vinahitaji ushahidi kutoka kwa wahusika.
Jaji
Shangali aliahirisha kesi hiyo mpaka kikao kingine cha mahakama kuu
kitakapoitwa ili ianze kusikilizwa.
Thursday, January 23, 2014
MAHABUSU AJIPAKA KINYESI KWA LENGO LA KUWATOROKA POLISI MKOANI MWANZA
Mahabusu mmoja
aliyekuwa mahabusu ya mahakama ya wilaya ya Nyamagana na Mahakama ya
Mwanzo iliyopo eneo la jirani na Mamlaka ya maji safi na Hifadhi ya
Mazingira (MWAUWASA) jijini Mwanza alitoa kioja cha mwaka kwa kujaribu
kutoroka kwa kujipaka kinyesi ili asiguswe wala kukamatwa.
Mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikufahamika alijimwagia kinyesi kilichokuwa kwenye ndoo iliyokuwa ndani ya sero ya Mahakamani hapo na askari alipokwenda kufungua ili kuwapeleka watuhumiwa kwenye chumba cha Mahakama kusomewa kesi yake baada ya kutajwa na karani wa Mahakama ya mwanzo, baada ya kutajwa ndipo mahabusu huyo alipopata mwanya wa kukimbia na kutoa tahadhari kwa atakaye mgusa au kumshika atakumbana na kadhia ya kuchafuliwa kwa kupakwa kinyesi.
Askari mwingine mwenye cheo cha sajenti, ambaye alikuwa akihushughulika na huduma nyingine mahakamani hapo, kwa kuwa alikuwa na uzoefu wa kupambana na mikasa na vioja kama hivyo vya mahabusu wanao kula njama za kutaka kutoroka aliamua kula naye sahani moja kwa kumkimbiza na kufanikiwa kumkamata.
Mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikufahamika alijimwagia kinyesi kilichokuwa kwenye ndoo iliyokuwa ndani ya sero ya Mahakamani hapo na askari alipokwenda kufungua ili kuwapeleka watuhumiwa kwenye chumba cha Mahakama kusomewa kesi yake baada ya kutajwa na karani wa Mahakama ya mwanzo, baada ya kutajwa ndipo mahabusu huyo alipopata mwanya wa kukimbia na kutoa tahadhari kwa atakaye mgusa au kumshika atakumbana na kadhia ya kuchafuliwa kwa kupakwa kinyesi.
Askari mwingine mwenye cheo cha sajenti, ambaye alikuwa akihushughulika na huduma nyingine mahakamani hapo, kwa kuwa alikuwa na uzoefu wa kupambana na mikasa na vioja kama hivyo vya mahabusu wanao kula njama za kutaka kutoroka aliamua kula naye sahani moja kwa kumkimbiza na kufanikiwa kumkamata.
Baada
ya kumkamata na kumrejesha katika chumba cha mahabusu mahakamani hapo,
kwanza mtuhumiwa huyo aliamriwa kuzoa mtondoro wa kinyesi cha binadamu
alichokuwa amejimwagia na kutapakaa chini na mara baada ya kumaliza
kuzoa uchafu huo, alipelekwa kwa hakimu ambapo alisomewa kosa la kula
njama za kutoroka na kukumbana na adhabu nyingine ya kuhukumiwa kifungo
cha miezi sita (6) jela, huku kesi yake iliyokuwa ikimkabili awali
ikiahirishwa.
Via Mzee wa matukio
Tuesday, December 31, 2013
WAFANYABIASHARA MWANZA WAZIGOMEA MASHINE ZA KIELETRONIKI (EFD)
"HATA BURE HATUZITAKI"
Shughuli za biashara ya maduka na huduma mbalimbali za kijamii katika jiji la Mwanza zimesimama kwa siku nzima kufuatia mgomo wa wafanyabiashara wakubwa na wa kati zaidi ya 2000, wanaopinga matumizi ya mashine za kodi za kielektroniki-EFD .
Ni sauti za wafanyabiashara wa jiji la Mwanza, wakiwa wamekusanyika katika kituo kikuu cha zamani cha mabasi cha stendi ya Tanganyika,
kilichopo katikati ya jiji la Mwanza, huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe unaoelezea namna wanavyonyanyasika kutokana na matumizi ya mashine hizo
Baadhi ya wafanyabiashara wakizungumza kwa jazba, wamesema hawako tayari kufanya biashara kwa kutumia mashine za TRA, hata kama watapewa bure kwa madai kwamba wengi wao bado ni wajasiriamali ambao mitaji yao bado ni midogo, huku wengine wakidai kwamba TRA haijawapa elimu kuhusu matumizi ya mashine hizo zaidi ya kuwapa muda wa kuanza kuzitumia
Mgomo huo, ambao umeathiri maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza na kusababisha usumbufu mkubwa kwa baadhi ya wakazi wa mikoa ya kanda ya ziwa, wanaotegemea kununua bidhaa mbalimbali kutoka katika maduka ya jumla yaliyopo jijini Mwanza, umemlazimu meneja wa mamlaka ya mapato ( TRA ) mkoa wa Mwanza Bw. Jeremiah Lusana pamoja na kaimu katibu tawala wa mkoa wa Mwanza Bw. Ndaro Kulwijila kuutolea tamko.
Friday, December 27, 2013
BREAKIN NEWZZZ!!- PICHA ZAKWANZA ZA THIS SUPER STAR MODEL MBONGO KUKAMATWA NA SEMBE MACAO/CHINA
Heroin drug packer arrested in Macao (2013-12-19)
A woman from Tanzania was arrested on a charge of drug possession in Macao, Dec 19, 2013. Police officers became suspicious of a female passenger who had flown from Thailand to Monaco on Tuesday (Dec,17,2013). The suspect, a tanzanian National, 28 was allegadly trying to smuggle drugs into Guangzhou. Guangzhou Proivence. After undergoing an X-ray scan, the suspect excreted 66 pellets of heroin, weighting 1.1 kilograms valued 1.1 millionMacao pataca ($137,755)
SUPER STAR DIAMOND PLATZNUM ALIPOMTANGAZA RASMI MCHUMBA WAKE MUPYA JANA LIVE!!
Ilikuwa jana pale Leaders club kwenye show ya Diamond ambapo Wema Sepetu alipanda kwenye stage na kuongea na mashabiki waliofika kwenye show hiyo.
Kwenye hiyo show Diamond aliuliza,”Mnataka kumjua mchumba wangu”?
Show ilivyoendelea Diamond alitaka kuimba wimbo wa ukimwona akasema, “Naskia ninayetaka kumuimbia wimbo huu yupo humuhumu ndani”.
Wema Sepetu akapanda kwenye stage wakaimba na kucheza wote.
Kwenye hiyo show Diamond aliuliza,”Mnataka kumjua mchumba wangu”?
Show ilivyoendelea Diamond alitaka kuimba wimbo wa ukimwona akasema, “Naskia ninayetaka kumuimbia wimbo huu yupo humuhumu ndani”.
Wema Sepetu akapanda kwenye stage wakaimba na kucheza wote.
Friday, December 20, 2013
MKALIMANI WA LUGHA YA ISHARA KATIKA SIKU YA MAZISHI YA MANDELA ALAZWA HOSPITALI YA MAGONJWA YA AKILI
MKALIMANI WA LUGHA YA ISHARA KATIKA SIKU YA MAZISHI YA MANDELA ALAZWA HOSPITALI YA MAGONJWA YA AKILI
Mkalimani wa lugha ya ishara katika siku ya mazishi ya kitaifa, ya aliyekuwa rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amelazwa katika hospitali ya magonjwa ya ya akili.
Mkalimani huyo anashutumiwa kutoa ishara ambazo hazikuendana na kile kilichokuwa kikiongelewa.
Thamsanqa Jantjie “anaweza kuwa na matatizo”, amekaririwa mke wake Siziwe akisema hayo.
Wataalam wa lugha ya ishara wamemshutumu kwa kutoa tafsiri potofu wakati viongozi mbalimbali wakitoa hotuba zao kwenye mazishi ya kitaifa ya Bwana Nelson Mandela wiki iliyopita.
Bwana Jantjie amesema aliumwa ghafla ugonjwa wa schizophrenia.
Amesisitiza kuwa alikuwa ni mkalimani mwenye ujuzi wa kazi hiyo.
Chama tawala cha African National Congress,ANC, amesema imekuwa ikimtumia Bwana Jantjie kama mkalimani wa lugha ya ishara katika matukio kadha siku za nyuma na hakuwahi kulalamikiwa kuhusiana na huduma yake, kwa upande wa ujuzi au maradhi yoyote.
Bwana Mandela alifariki dunia tarehe 5 Desemba mwaka huu akiwa na umri wa miaka 95 na kuzikwa Jumapili.
Thamsanqa Jantjie “anaweza kuwa na matatizo”, amekaririwa mke wake Siziwe akisema hayo.
Wataalam wa lugha ya ishara wamemshutumu kwa kutoa tafsiri potofu wakati viongozi mbalimbali wakitoa hotuba zao kwenye mazishi ya kitaifa ya Bwana Nelson Mandela wiki iliyopita.
Bwana Jantjie amesema aliumwa ghafla ugonjwa wa schizophrenia.
Amesisitiza kuwa alikuwa ni mkalimani mwenye ujuzi wa kazi hiyo.
Chama tawala cha African National Congress,ANC, amesema imekuwa ikimtumia Bwana Jantjie kama mkalimani wa lugha ya ishara katika matukio kadha siku za nyuma na hakuwahi kulalamikiwa kuhusiana na huduma yake, kwa upande wa ujuzi au maradhi yoyote.
Bwana Mandela alifariki dunia tarehe 5 Desemba mwaka huu akiwa na umri wa miaka 95 na kuzikwa Jumapili.
via Kibs 24
Subscribe to:
Posts (Atom)



















