Pages

Thursday, February 13, 2014

KESI YA DAUDI MWANGOSI YAANZA KUSIKILIZWA


 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa, Frank Leonard ( wa nne kushoto mwenye begi ndogo begani) akiwa nje ya mahakama kuu kanda ya Iringa na wanahabari wengine mara baada ya kesi ya mtuhumiwa wa mauaji ya Daudi Mwangnosi kusikilizwa




Waandishi wakisubiri kupiga picha ya mtuhumiwa bila mafanikio hadi wanaondoka eneo la tukio (mahakamani)

KESI ya mauaji ya aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Channel Ten Mkoani Iringa, Daudi Mwangosi imeanza kusikilizwa hii leo baada ya kilichoelezwa na upande wa mashtaka kwamba uchunguzi wake umakamilika.

Kama ilivyo ada, makechero wa Polisi wengi wao wakiwa wamavaa kiraia walikuwepo mahakamani hapa huku wakijaribu kuwazuia wanahabari kutekeleza wajibu wao.

Katika mazingira ya kutatanisha, mwandishi wa habari wa gazeti la Habarileo, Frank Leonard ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa alikamatwa na askari wanne waliokuwa wamevaa kiraia kwa kile kilichoelezwa kwamba alikuwa akipiga picha mahakamani wakati kesi ikiendele
Baada ya kukamatwa Leonard, alifikishwa kituo cha Polisi cha Kati mjini Iringa na kuachiwa huru baada ya kukosekana ushahidi.

Akizungumza na wanahabari baada ya kuachiwa huru, Leonard alisema "wapo baadhi ya askari kwa makusudi wanataka kubomoa mahusiano baina ya wanahabari na jeshi la Polisi ambayo yanaendelea kujengwa na kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi."


Alisema kitendo cha kubambikiziwa tuhuma ndani ya muhimili wa dola unaojitegemea (mahakama) ni kitendo cha uzalilishaji kinachotaka kuaminisha umma kwamba wanahabari ni watu wasiotaka kufuata taratibu za kimahakama.

Alisema akiwa ndani ya chumba cha mahakama hiyo alikamatwa na askari hao bila idhini ya Jaji wa Mahakama Kuu wakati akizima simu yake ya mkononi iliyokuwa katika mtetemo.


"Nilikuwa nazima simu yangu hao askari hao kwasababu wanazojua wao wenyewe waligeuza suala hilo ili lionekane katika sura wanayoitaka na hatimaye wanifungulie mashtaka," alisema.


Alimshukuru Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Iringa, Ngoi kwa kumtendea haki na baada ya kupata ushahidi kufutilia mbali kesi hiyo.

Akizungumza na wanahabari, Msajili wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Dunstan Nduguru aliwashangaa Polisi kwa kuingia shughuli za mahakama.

"Hata kama mwandishi huyo angekuwa anapiga picha, haikuwa kazi yao kumkamata mpaka wapewe agizo na Jaji Mfawidhi aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo," alisema.

Pamoja na askari hao kuwazuia wanahabari kuchukua picha mara baada ya mtuhumiwa huyo kufikishwa mahakamani, Nduguru alisema utaratibu wa mahakama unawaruhusu wanahabari kuchukua picha kabla shughuli kabla shughuli za mahakama hazijaanza na baada ya shughuli hizo kwisha.

"Kuwazuia wanahabari kufanya kazi zao kwa utaratibu huo sio sahihi; siku nyingine mkiona kuna dalili ya kupata bugudha kama hiyo naomba mnijulishe ili niondoe mzozo huo," alisema. 

Mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Mary Shangali, Wakili wa upande wa mashtka, Adolph Maganga alisema Adolph Maganda alisema kwa kukusudia mtuhumiwa Pacificius Cleophace Simoni anatuhumiwa kumuua Mwangosi kinyume na kifungu cha sheria ya kanuni ya adhabu namba 196 sura ya 16 kilichofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Alisema katika tukio hilo lililotokea Septemba 2, 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa, mshtakiwa alifyatua bunduki yake na kusababisha kifo cha marehemu, papo hapo.

Alisema siku ya tukio marehemu alikuwa Nyororo kwa ajili ya kuripoti na kutoa taarifa kwa umma juu ya mkutano uliokuwa ufanywe na katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Alisema mshtakiwa akiwa mmoja wa wafanyakazi wa Polisi, waliwasihi Chadema wasifanye mkutano huo kabla wafuasi wake hawajaanza kurusha mawe kwa Polisi na baadhi yao kupata majeraha.

Kutokana na mzozo huo, wakili huyo wa serikali alisema polisi walipiga mabomu ya machozi ili kuwatawanya wafuasi hao kabla mshtakiwa huyo hajamfyatulia bomu marehemu.

Wakili huyo aliwasilisha ramani ya eneo la tukio, ripoti ya mtaalamu wa milipuko na ripoti ya daktari aliyechunguza mwili wa marehemu Mwangosi na gazeti la Mwananchi la Septemba 3, 2012 lililochapisha  picha ya tukio hilo katika ukurasa wa mbele kama vielelezo vinavyohusiana na kesi hiyo.

Wakili wa upande wa utetezi Lwezaula Kaijage alitaja mambo wanayokubaliana katika kesi hiyo kuwa ni jina na anuani ya mshtakiwa na kwamba marehemu Mwangosi alikufa kifo ambacho si cha kawaida.

Na kwamba mshtakiwa Simoni alikamatwa na amefikishwa mahakamani akihusishwa na mauaji hayo.

Wakili Kaijage alisema vielelezo vingine vilivyoletwa na upande wa mashtaka hawakubaliani navyo kwakuwa vinahitaji ushahidi kutoka kwa wahusika.
Jaji Shangali aliahirisha kesi hiyo mpaka kikao kingine cha mahakama kuu kitakapoitwa ili ianze kusikilizwa.

Thursday, January 23, 2014

MAHABUSU AJIPAKA KINYESI KWA LENGO LA KUWATOROKA POLISI MKOANI MWANZA

 




 Mahabusu mmoja aliyekuwa mahabusu ya mahakama ya wilaya ya Nyamagana na Mahakama ya Mwanzo iliyopo eneo la jirani na Mamlaka ya maji safi na Hifadhi ya Mazingira (MWAUWASA) jijini Mwanza alitoa kioja cha mwaka kwa kujaribu kutoroka kwa kujipaka kinyesi ili asiguswe wala kukamatwa.

Mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikufahamika alijimwagia kinyesi kilichokuwa kwenye ndoo iliyokuwa ndani ya sero ya Mahakamani hapo na askari alipokwenda kufungua ili kuwapeleka watuhumiwa kwenye chumba cha Mahakama kusomewa kesi yake baada ya kutajwa na karani wa Mahakama ya mwanzo, baada ya kutajwa ndipo mahabusu huyo alipopata mwanya wa kukimbia na kutoa tahadhari kwa atakaye mgusa au kumshika atakumbana na kadhia ya kuchafuliwa kwa kupakwa kinyesi.

Askari mwingine mwenye cheo cha sajenti, ambaye alikuwa akihushughulika na huduma nyingine mahakamani hapo, kwa kuwa alikuwa na uzoefu wa kupambana na mikasa na vioja kama hivyo vya mahabusu wanao kula njama za kutaka kutoroka aliamua kula naye sahani moja kwa kumkimbiza na kufanikiwa kumkamata.


Baada ya kumkamata na kumrejesha katika chumba cha mahabusu mahakamani hapo, kwanza mtuhumiwa huyo aliamriwa kuzoa mtondoro wa kinyesi cha binadamu alichokuwa amejimwagia na kutapakaa chini na mara baada ya kumaliza kuzoa uchafu huo, alipelekwa kwa hakimu ambapo alisomewa kosa la kula njama za kutoroka na kukumbana na adhabu nyingine ya kuhukumiwa kifungo cha miezi sita (6) jela, huku kesi yake iliyokuwa ikimkabili awali ikiahirishwa.
Via Mzee wa matukio

Tuesday, December 31, 2013

WAFANYABIASHARA MWANZA WAZIGOMEA MASHINE ZA KIELETRONIKI (EFD)

"HATA BURE HATUZITAKI"

Shughuli za biashara ya maduka na huduma mbalimbali za kijamii katika jiji la Mwanza zimesimama kwa siku nzima kufuatia mgomo wa wafanyabiashara wakubwa na wa kati zaidi ya 2000, wanaopinga matumizi ya mashine za kodi za kielektroniki-EFD .

Ni sauti za wafanyabiashara wa jiji la Mwanza, wakiwa wamekusanyika katika kituo kikuu cha zamani cha mabasi cha stendi ya Tanganyika,

 kilichopo katikati ya jiji la Mwanza, huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe unaoelezea namna wanavyonyanyasika kutokana na matumizi ya mashine hizo

Baadhi ya wafanyabiashara wakizungumza kwa jazba, wamesema hawako tayari kufanya biashara kwa kutumia mashine za TRA, hata kama watapewa bure kwa madai kwamba wengi wao bado ni wajasiriamali ambao mitaji yao bado ni midogo, huku wengine wakidai kwamba TRA haijawapa elimu kuhusu matumizi ya mashine hizo zaidi ya kuwapa muda wa kuanza kuzitumia



Mgomo huo, ambao umeathiri maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza na kusababisha usumbufu mkubwa kwa baadhi ya wakazi wa mikoa ya kanda ya ziwa, wanaotegemea kununua bidhaa mbalimbali kutoka katika maduka ya jumla yaliyopo jijini Mwanza, umemlazimu meneja wa mamlaka ya mapato ( TRA ) mkoa wa Mwanza Bw. Jeremiah Lusana pamoja na kaimu katibu tawala wa mkoa wa Mwanza Bw. Ndaro Kulwijila kuutolea tamko.


Via ITV

Friday, December 27, 2013

BREAKIN NEWZZZ!!- PICHA ZAKWANZA ZA THIS SUPER STAR MODEL MBONGO KUKAMATWA NA SEMBE MACAO/CHINA

Heroin drug packer arrested in Macao (2013-12-19) 
A woman from Tanzania was arrested on  a charge of drug possession in Macao, Dec 19, 2013. Police officers became suspicious of a female passenger who had flown from Thailand to Monaco on Tuesday (Dec,17,2013). The suspect, a tanzanian National, 28 was allegadly trying to smuggle drugs into Guangzhou. Guangzhou Proivence. After undergoing an X-ray scan, the suspect excreted 66 pellets of heroin, weighting 1.1 kilograms valued 1.1 millionMacao pataca ($137,755)







SUPER STAR DIAMOND PLATZNUM ALIPOMTANGAZA RASMI MCHUMBA WAKE MUPYA JANA LIVE!!


Ilikuwa jana pale Leaders club kwenye show ya Diamond ambapo Wema Sepetu alipanda kwenye stage na kuongea na mashabiki waliofika kwenye show hiyo.
Kwenye hiyo show Diamond aliuliza,”Mnataka kumjua mchumba wangu”?
Show ilivyoendelea Diamond alitaka kuimba wimbo wa ukimwona akasema, “Naskia ninayetaka kumuimbia wimbo huu yupo humuhumu ndani”.
Wema Sepetu akapanda kwenye stage wakaimba na kucheza wote.







Friday, December 20, 2013

MKALIMANI WA LUGHA YA ISHARA KATIKA SIKU YA MAZISHI YA MANDELA ALAZWA HOSPITALI YA MAGONJWA YA AKILI


MKALIMANI WA LUGHA YA ISHARA KATIKA SIKU YA MAZISHI YA MANDELA ALAZWA HOSPITALI YA MAGONJWA YA AKILI

Mkalimani huyo anashutumiwa kutoa ishara ambazo hazikuendana na kile kilichokuwa kikiongelewa.
Thamsanqa Jantjie “anaweza kuwa na matatizo”, amekaririwa mke wake Siziwe akisema hayo.
Wataalam wa lugha ya ishara wamemshutumu kwa kutoa tafsiri potofu wakati viongozi mbalimbali wakitoa hotuba zao kwenye mazishi ya kitaifa ya Bwana Nelson Mandela wiki iliyopita.
Bwana Jantjie amesema aliumwa ghafla ugonjwa wa schizophrenia.
Amesisitiza kuwa alikuwa ni mkalimani mwenye ujuzi wa kazi hiyo.
Chama tawala cha African National Congress,ANC, amesema imekuwa ikimtumia Bwana Jantjie kama mkalimani wa lugha ya ishara katika matukio kadha siku za nyuma na hakuwahi kulalamikiwa kuhusiana na huduma yake, kwa upande wa ujuzi au maradhi yoyote.
Bwana Mandela alifariki dunia tarehe 5 Desemba mwaka huu akiwa na umri wa miaka 95 na kuzikwa Jumapili.

via Kibs 24

Tuesday, December 17, 2013

WASICHANA WAWILI WADAKWA NA DAWA ZA KULEVYA UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU NYERERE



Kamanda Godfrey Nzoa

Polisi imewakamata wasichana wawili wa Kitanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam, wakiwa na zaidi ya pipi 187 za madawaya kulevya   walizokuwa wamezimeza  kwa ajili ya kusafirisha nchini China.

Aidha, polisi imemtia mbaroni, raia wa China Guoyn Shen (44), kwa kukutwa na madini aina ya quates kilo 19 aliyokuwa akiyasafirisha kwa njia ya ndege kuelekea China.


Wasichana waliokamatwa Jumatano ya wiki hii saa 11:00 jioni. uwanjani hapo walikuwa kwenye harakati za kupanda ndege ya kampuni ya ndege ya Qatar kuelekea China kupitia Hong Kong.

Kwa mujibu wa Mkuu wa kitengo cha kupambana na dawa za kulevya, nchini Kamanda Godfrey Nzoa, wasichana hao ni Mariam Makuhani (29) mkazi wa Tabata Kimanga  na Khadija Shomari (30), mkazi wa Magomeni Mapipa ambao hadi jana asubuhi walikuwa wanaendelea kuzitoa pipi hizo kwa njia ya haja kubwa.
Alisema Mariam kwa wakati huo (saa 5:00) alikuwa ametoa pipi 65  wakati Khadija alifanikiwa kutoa pipi 122 ambazo zitapelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kubaini ni za aina gani na thamani yake.

Alisema wasichana hao bado wapo chini ya uangalizi ambapo baada ya kumaliza zoezi hilo wataandaliwa mashitaka yao na kufikishwa mahakamani kujibu makosa yanayowakabili.

Kaimu wa Viwanja vya Ndege nchini, Mratibu wa polisi, Renatus Chalya, alisema awali baada ya wasichana hao kukamatwa, Mariam alikiri kumeza pipi 72 huku Khadija akidai alimsindikiza Mariam.


Akizungumzia changamoto za kupambana na madawa ya kulevya, Kamanda Nzoa alisema wasafirishaji wamekuwa wakiibuka na mbinu tofauti na wengine wakisafirisha viatilifu vya kutengenezea dawa hizo badala ya dawa zenyewe.

Alisema mbinu hizo zimekuwa zikifanywa kwa msimu na kutaja njia ambazo hutumiwa kuwa ni majini, viwanja vya ndege na nchi kavu.

Kufuatia changamoto hiyo, Tanzania na nchi nyingine duniani zilishiriki mikutano mbalimbali ambapo wa mwisho ulifanyika mwezi Oktoba mwaka huu nchini Afrika Kusini.

Alisema katika mkutano huo washiriki pamoja na mambo mengine walipata fursa ya kueleza changamoto wanazokabiliana nazo kwenye mapambano dhidi ya dawa hizo ambapo lililojitokeza ni usafirishaji wa viatilifu.


"Tuliliongelea kwa upana wake suala hili na kuafikiana kuwepo kwa sheria kali kwa kuwa tunayoitumia kwa mfano Tanzania haiwabani sana," alisema na kuongeza:
Alisema nchi zilizoshiriki mkutano huo zilibaini hiyo ni moja ya changamoto hivyo wakakubaliana kutungwe sheria itakayokuwa na makali zaidi.


Kamanda Nzoa aliwataja Watanzania wawili waliokamatwa kwa nyakati tofauti na viatilifu Agnes Masogange, Afrika Kusini na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Sada  aliyekamatwa Tanzania ambao kutokana na sheria hiyo walilipa faini ndogo na kuachiwa huru.


Alisema sheria iliyopo inatoa nguvu kwa mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ambapo mtu akikamatwa na viatilifu hivyo bila kibali atachukuliwa hatua za kisheria.
Kamanda Nzoa alisema kuanzia mwezi Machi hadi Julai mwaka huu, wamefanikiwa kukamata kilo 1482 ambazo tayari zilishaharibiwa.


Alisema dawa hizo zilikamatwa kwa nyakati tofauti kwenye meli ambapo moja ilikutwa na kilo 500, nyingine kilo 300.

"Ipo iliyokutwa na kilo 200 meli nyingine ilikutwa na kilo 182 ambapo hata hivyo kutokana na eneo walilokutwa walishindwa kuwafikisha mahakamani badala yake waliharibu mzigo huo," alisema.

Kwa upande wa njia ya anga, alisema kwa mwaka huu wamefanikiwa kukamata kilo 50 bila kuzijumlisha zinazoendelea kutolewa na wasichana hao wawili waliokamatwa Jumatano.

"Ipo kesi ambayo ukija hapa ofisi kwangu nitakuonyesha mlolongo mzima, huwezi amini tulikamata watu tena wakazitoa dawa hizo kwa njia ya haja kubwa lakini mahakama iliwaachilia, kama nilivyosema tunapoenda mahakamani tunatakiwa kuthibitisha pasipo kuacha shaka," alisema.

Kamanda Nzoa alisema kutokana na changamoto hizo, tayari wameshawapeleka vijana wao nchi mbalimbali na kutaja baadhi kuwa ni Afrika Kusini, Ghana, India, Iran, Ivory Cost  kwa ajili ya mafunzo maalum.

Kuhusu Mchina aliyekamatwana madini alisema kuwa Shen alikamatwa Jumatano wiki hii uwanjani hapo akiwa kwenye harakati za kusafirisha mzigo huo kuelekea nchini humo.

Alisema mtuhumiwa huyo alikuwa akisafiri na ndege ya kampuni ya ndege ya Ethiopia iliyokuwa iondoke jioni ya siku hiyo.

Alisema mtuhumiwa huyo alipokamatwa alipotakiwa kutoa kibali cha kusafirisha mzigo huo hakuwa nacho na alipoulizwa ameyapata wapi alidai ameyanunua kwa wananchi.


Alitaja namba za hati ya kusafiria ya mtuhumiwa huyo kuwa ni 00609687.Alisema upelelezi wa tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na kubaini thamani ya madini hayo.

VIA Nipashe