Wednesday, November 28, 2012
Tuesday, November 27, 2012
Monday, November 26, 2012
SHARO MILLIONEA AFARIKI KATIKA AJALI
AMAKWELI UDONGO UNAFAIDI
Kuna habari za kusikitisha na uhakika kuwa msanii aliyekuwa maarufu kwa jina la Sharo Millionea, msanii wa muziki na maarufu katika kuwepo kwake katika matangazo kwa style ya aina yake amefariki dunia baada ya kupata ajali ya gari Tanga.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi
Wednesday, November 21, 2012
VIJANA WA UMRI KATI 20 NA 45 KUTOJITOKEZA KUPATA HUDUMA YA TOHARA
Na Mercy Mwalusamba
Iringa
Iringa
Huduma ya tohara inayoendelea kutolewa katika hospitali ya mkoa wa Iringa imekuwa na mafanikio katika kipindi cha mwaka 2010 – 2011 kufuatia kampeni maalumu ya dondosha mkono sweta
Akizungumza na waandishi wa habari jana Muuguzi wa hospitali ya Mkoa katika kitengo cha upasuaji Iluminata Sanga alisema kabla ya mpango wa serikali juu ya huduma ya tohara na uhamasishaji katika kampeni ya dondosha mkono sweta, hali ya wananchi waliopata huduma hiyo ilikua chini kwa asilimia 35
Alisema baada ya mpango mkakati kuanza mwaka 2010 huduma imetolewa kwa mpango maalumu kupitia hospitali ya mkoa pamoja na vituo vya afya vya Ngome manispaa,hospitali ya Tosamaganga Mufindi na Lugoda ambapo jumla ya watu waliopata huduma ni 10,302 hadi sasa
Huduma ya tohara imefanyika kwa kiwango kikubwa vijijini ikilinganishwa na mjini ambapo wengi wao ni watoto kati ya umri 10 hadi 14 na 15 hadi 20 idadi iliyofikia asilimia 65 alisema Sanga
Sanga alisema hali ya usafi kwa mtu aliefanyiwa tohara ndio jambo la msingi kwani bila kua na hali ya usafi katika kidonda husababisha madhara na kidonda kutokupona haraka
“Watu wanaokuja kupata huduma wamekuwa wakipewa elimu ya ushauri nasaha na upimaji wa afya kwakuzingatia vipimo muhimu ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea baada ya tohara” alisema
Aliongeza kuwa kumekuwa na baadhi ya watoto wenye umri chini ya miaka 18 ambao hufika peke yao kupata huduma hii bila wazazi wao au walezi kinyume na utaratibu kwani huduma kwa watoto wa umri huo hutolewa chini ya uangalizi na usimamizi wa wazazi
Alisema kuna haja ya kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na tohara ili kuepukana na changamoto zilizojitokeza kama kufikiri kufanyiwa tohara ni kuruhusu kuendelea kufanya vitendo vya ngono au kupunguza nguvu za kiume
“tohara inamsaidia mtu kuishi katika mazingira salama ya kupunguza uwezekano wa maabukizi ya magonjwa ya ngono”
……………………….MWISHO……………………..
Subscribe to:
Posts (Atom)










