Tuesday, November 27, 2012
Monday, November 26, 2012
SHARO MILLIONEA AFARIKI KATIKA AJALI
AMAKWELI UDONGO UNAFAIDI
Kuna habari za kusikitisha na uhakika kuwa msanii aliyekuwa maarufu kwa jina la Sharo Millionea, msanii wa muziki na maarufu katika kuwepo kwake katika matangazo kwa style ya aina yake amefariki dunia baada ya kupata ajali ya gari Tanga.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi
Wednesday, November 21, 2012
VIJANA WA UMRI KATI 20 NA 45 KUTOJITOKEZA KUPATA HUDUMA YA TOHARA
Na Mercy Mwalusamba
Iringa
Iringa
Huduma ya tohara inayoendelea kutolewa katika hospitali ya mkoa wa Iringa imekuwa na mafanikio katika kipindi cha mwaka 2010 – 2011 kufuatia kampeni maalumu ya dondosha mkono sweta
Akizungumza na waandishi wa habari jana Muuguzi wa hospitali ya Mkoa katika kitengo cha upasuaji Iluminata Sanga alisema kabla ya mpango wa serikali juu ya huduma ya tohara na uhamasishaji katika kampeni ya dondosha mkono sweta, hali ya wananchi waliopata huduma hiyo ilikua chini kwa asilimia 35
Alisema baada ya mpango mkakati kuanza mwaka 2010 huduma imetolewa kwa mpango maalumu kupitia hospitali ya mkoa pamoja na vituo vya afya vya Ngome manispaa,hospitali ya Tosamaganga Mufindi na Lugoda ambapo jumla ya watu waliopata huduma ni 10,302 hadi sasa
Huduma ya tohara imefanyika kwa kiwango kikubwa vijijini ikilinganishwa na mjini ambapo wengi wao ni watoto kati ya umri 10 hadi 14 na 15 hadi 20 idadi iliyofikia asilimia 65 alisema Sanga
Sanga alisema hali ya usafi kwa mtu aliefanyiwa tohara ndio jambo la msingi kwani bila kua na hali ya usafi katika kidonda husababisha madhara na kidonda kutokupona haraka
“Watu wanaokuja kupata huduma wamekuwa wakipewa elimu ya ushauri nasaha na upimaji wa afya kwakuzingatia vipimo muhimu ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea baada ya tohara” alisema
Aliongeza kuwa kumekuwa na baadhi ya watoto wenye umri chini ya miaka 18 ambao hufika peke yao kupata huduma hii bila wazazi wao au walezi kinyume na utaratibu kwani huduma kwa watoto wa umri huo hutolewa chini ya uangalizi na usimamizi wa wazazi
Alisema kuna haja ya kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na tohara ili kuepukana na changamoto zilizojitokeza kama kufikiri kufanyiwa tohara ni kuruhusu kuendelea kufanya vitendo vya ngono au kupunguza nguvu za kiume
“tohara inamsaidia mtu kuishi katika mazingira salama ya kupunguza uwezekano wa maabukizi ya magonjwa ya ngono”
……………………….MWISHO……………………..
MTUHUMIWA WA MAUAJI YA MWANGOSI AFIKISHWA MAHAKAMANI TENA
Na mercy Mwalusamba
Iringa
Iringa
MTUHUMIWA wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha runinga cha Channel Ten Daud Mwangosi alifikishwa mahakamani jana katika ulinzi mkali huku waandishi wa habari wakiendelea kuzuiwa na polisi kupiga picha.
Askari wa kikosi cha kuzuia ghasia wengine waliokuwa na silaha mbalimbali huku wengine wakivaa kiraia waliweka ulinzi mkali kuhakikisha waandishi wa habari hawapati mwanya wa kupiga picha.
Mwendesha mashtaka wa serikali Adolf Maganda aliambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Dyness Lyimo kuwa upelelezia wa kesi hiyo haujakamilia.
Pasificus Cleophace Simon (23) alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa tuhuma ya kumuua kwa makusudi mwandishi huyo katika ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa uliofanyika Septemba 2 mwaka huu.
Mtuhumiwa huyo mwenye namba G 2573 alifikishwa mahakamani hapo kwa
gari la polisi lenye namba PT 1404 likiwa na ulinzi mkali akiwa amefichwa uso kiasi cha kutoonekana macho yake.
Siku ya kwanza mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo kwa gari la kifahari lenye namba za kiraia T 320 ARC linalosadikiwa kuwa ni la RCO huku kwa mara ya pili akifikishwa kwa miguu na kuondolewa mahakamani hapo kwa gari namba DFP 2175 pick up akiwa katika ulinzi mkali huku waandishi wa habari wakidhibitiwa na polisi na mmoja wao kunusurika kupigwa jambo lililozusha hisia tofauti miongoni mwa wananchi wengi mkoani hapa.
Kwa mujibu wa wakili huyo, upelelezi haujakamilika na kesi imeahirishwa hadi Desemba 05 mwaka huu itakapotajwa tena.
Unyanyaswaji wa waandishi wa habari wakati wa kupiga picha za mtuhumiwa wa mauaji hayo unaendelea kushika kasi baada ya mwandishi wa gazeti Tanzania daima kupigwa na askari kanzu kwenye chumba cha mahakama alipotaka kupiga picha kabla ya mahakama kuanza jambo ambalo limelaaniwa vikali na waandishi pamoja na wananchi waliokuwepo mahakamani hapo.
Askari wa kikosi cha kuzuia ghasia wengine waliokuwa na silaha mbalimbali huku wengine wakivaa kiraia waliweka ulinzi mkali kuhakikisha waandishi wa habari hawapati mwanya wa kupiga picha.
Mwendesha mashtaka wa serikali Adolf Maganda aliambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Dyness Lyimo kuwa upelelezia wa kesi hiyo haujakamilia.
Pasificus Cleophace Simon (23) alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa tuhuma ya kumuua kwa makusudi mwandishi huyo katika ufunguzi wa matawi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa uliofanyika Septemba 2 mwaka huu.
Mtuhumiwa huyo mwenye namba G 2573 alifikishwa mahakamani hapo kwa
gari la polisi lenye namba PT 1404 likiwa na ulinzi mkali akiwa amefichwa uso kiasi cha kutoonekana macho yake.
Siku ya kwanza mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo kwa gari la kifahari lenye namba za kiraia T 320 ARC linalosadikiwa kuwa ni la RCO huku kwa mara ya pili akifikishwa kwa miguu na kuondolewa mahakamani hapo kwa gari namba DFP 2175 pick up akiwa katika ulinzi mkali huku waandishi wa habari wakidhibitiwa na polisi na mmoja wao kunusurika kupigwa jambo lililozusha hisia tofauti miongoni mwa wananchi wengi mkoani hapa.
Kwa mujibu wa wakili huyo, upelelezi haujakamilika na kesi imeahirishwa hadi Desemba 05 mwaka huu itakapotajwa tena.
Unyanyaswaji wa waandishi wa habari wakati wa kupiga picha za mtuhumiwa wa mauaji hayo unaendelea kushika kasi baada ya mwandishi wa gazeti Tanzania daima kupigwa na askari kanzu kwenye chumba cha mahakama alipotaka kupiga picha kabla ya mahakama kuanza jambo ambalo limelaaniwa vikali na waandishi pamoja na wananchi waliokuwepo mahakamani hapo.
Mwangosi aliuawa kwa bomu Septemba 2 mwaka huu katika kijiji cha Nyololo yo alipokuwa akiwajibika kwa kazi za kihabari wakati wa ufunguzi wa matawi hayo.
………………………………………………. Mwisho ………………………………………..
Saturday, November 17, 2012
WANNE MBARONI KUFUATIA TUKIO LA UVAMIZI PAROKIA YA ISIMANI IRINGA
Na Mercy Mwalusamba
Iringa
Kutokana na sakata la mapadre wa Parokia ya Isimani Jimbo Katoliki la
Iringa kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, watu
wanne wametiwa mbaroni wakituhumiwa kuhusika na tukiohilo .
Hii inakuja siku moja baada ya mapare wawili wa Parokia hiyo kuvamiwa
nyumbani kwao na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimba za mwili kwa
silaha.
Siku moja kabla ya kuvamiwa mapadre hao watu wasiojulikana walivamia
mlinzi wa Kanisa katika Parokia ya Kihesa na kumjeruhi vibaya na kitu
kizito kichwani ndipo walipovunja milango ya Kanisa na kuiba pesa
kadhaa, baadhi ya vyombo vya ibada na kuharibu vibaya mavazi ya ibada,
vitabu na nyaraka mbalimbali kiasi cha kutotamanika tena.
Miongoni mwa vyombo vya ibada vilivyoharibiwa na watu hao ni pamoja na
Kuvunjwa Msalaba, Monstranti, Taberenakulo ndogo pamoja na kumwagwa
ovyo Hostia Takatifu.
Usiku wa kuamkia juzi watu wanaokadiriwa kufikia saba wakiwa na
bunduki, rungu na mapanga walivamia makazi ya mapadri hao majira ya
saa nne za usiku, ambapo walimpiga nne Padre Angelo Burgio ambaye ni
Paroko wa Parokia hiyo na kumjeruhi vibaya msaidizi wake Pd. Helman
Myala fedha zaidi ya shilingi 3.9 milioni na Euro 100.
Watuhumiwa waliokamatwa kuhisiana na tukiohilo wametajwa kuwa ni
Joseph Ngwale (30), Erasto Ngwale (38), Gaitan Kitwange na Anita
Mwinuka wote wakazi wa Isimani.
Taarifa kutoka kwa wananchi mmoja wa kijiji hicho mshiriki wa msako
huo ambaye alitoa taarifa hizi wa masharti ya kutataka jina lake
liandikwe alisema kuwa ,walianza kupata watuhumiwa baada ya kufanya
upekuzi katika nyumba ya Josepha Ngwale na kupata goroli 37 na gram
100 huku ikipatikana silaha gobore iliyotumika katika ujambazi huo
ambayo kwa usiku huo ililetwa na mwanye Joseph Ngwale ili aifiche.
Tarifa hizo zilithibitishwa na Diwani wa Kata ya Kihorogota
Costantino Kihwele ambaye alisema watuhumiwa wote wamekwisha
kufikishwa polisi ili hatua za kisheria zifuate.
Hata hivyo watuhumiwa hao wamekiri kuhusika na tukio la uvamizi wa
Kanisa Kuu la kiaskofu Parokia ya Kihesa.
Kaimu wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dk. Gwanchele Faustine alisema baada ya
kumfanyia upasuaji Pd. Angelo waliweza kutoa risasi 3 sehemu ya
kifuani ambazo zilikuwa zimekwama na kueleza kuwa hali zao zinaendelea
kuimarika.
“Jana tulimfanyia upasuaji Pd. Angelo tukaweza kutoa risasi 3 sehemu
ya kifuani ambazo zilikuwa zimekwama. Hali zao zinaendelea kuimarika
huku tukifanya jitihada za kuwahudumia” alisema Dk. Faustine.
Katika hatua nyingine Dk. Faustine alisema kuwa Mlinzi wa Kanisa la
Kihesa Bathlomeo Nzigilwa aliyejeruhiwa na watu hao bado hali yake ni
mbaya japo kuwa kuna dalili za kuweza hata kufumbua macho.
“Mlinzi wa Kanisa la Kihesa aliyejeruhiwa na kuletwa hapa hospitalini
bado hali yake ni mbaya na tumegundua kuwa alivunjika mfupa wa
kichwani kwa hiyo tunaendelea kufanya utaratibu wa kuutoa. Ila kwa leo
amekuwa na dalili za kufumbua macho kwa hiyo tunafanya jitihada za
kumpa huduma zaidi” alisema Dk. Faustine.
…………………………………….. Mwisho ……………………………
Iringa kupigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, watu
wanne wametiwa mbaroni wakituhumiwa kuhusika na tukio
Hii inakuja siku moja baada ya mapare wawili wa Parokia hiyo kuvamiwa
nyumbani kwao na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimba za mwili kwa
silaha.
Siku moja kabla ya kuvamiwa mapadre hao watu wasiojulikana walivamia
mlinzi wa Kanisa katika Parokia ya Kihesa na kumjeruhi vibaya na kitu
kizito kichwani ndipo walipovunja milango ya Kanisa na kuiba pesa
kadhaa, baadhi ya vyombo vya ibada na kuharibu vibaya mavazi ya ibada,
vitabu na nyaraka mbalimbali kiasi cha kutotamanika tena.
Miongoni mwa vyombo vya ibada vilivyoharibiwa na watu hao ni pamoja na
Kuvunjwa Msalaba, Monstranti, Taberenakulo ndogo pamoja na kumwagwa
ovyo Hostia Takatifu.
Usiku wa kuamkia juzi watu wanaokadiriwa kufikia saba wakiwa na
bunduki, rungu na mapanga walivamia makazi ya mapadri hao majira ya
saa nne za usiku, ambapo walimpiga nne Padre Angelo Burgio ambaye ni
Paroko wa Parokia hiyo na kumjeruhi vibaya msaidizi wake Pd. Helman
Myala fedha zaidi ya shilingi 3.9 milioni na Euro 100.
Watuhumiwa waliokamatwa kuhisiana na tukio
Joseph Ngwale (30), Erasto Ngwale (38), Gaitan Kitwange na Anita
Mwinuka wote wakazi wa Isimani.
Taarifa kutoka kwa wananchi mmoja wa kijiji hicho mshiriki wa msako
huo ambaye alitoa taarifa hizi wa masharti ya kutataka jina lake
liandikwe alisema kuwa ,walianza kupata watuhumiwa baada ya kufanya
upekuzi katika nyumba ya Josepha Ngwale na kupata goroli 37 na gram
100 huku ikipatikana silaha gobore iliyotumika katika ujambazi huo
ambayo kwa usiku huo ililetwa na mwanye Joseph Ngwale ili aifiche.
Tarifa hizo zilithibitishwa na Diwani wa Kata ya Kihorogota
Costantino Kihwele ambaye alisema watuhumiwa wote wamekwisha
kufikishwa polisi ili hatua za kisheria zifuate.
Hata hivyo watuhumiwa hao wamekiri kuhusika na tukio la uvamizi wa
Kanisa Kuu la kiaskofu Parokia ya Kihesa.
Kaimu wa Mganga Mkuu wa Mkoa Dk. Gwanchele Faustine alisema baada ya
kumfanyia upasuaji Pd. Angelo waliweza kutoa risasi 3 sehemu ya
kifuani ambazo zilikuwa zimekwama na kueleza kuwa hali zao zinaendelea
kuimarika.
“Jana tulimfanyia upasuaji Pd. Angelo tukaweza kutoa risasi 3 sehemu
ya kifuani ambazo zilikuwa zimekwama. Hali zao zinaendelea kuimarika
huku tukifanya jitihada za kuwahudumia” alisema Dk. Faustine.
Katika hatua nyingine Dk. Faustine alisema kuwa Mlinzi wa Kanisa la
Kihesa Bathlomeo Nzigilwa aliyejeruhiwa na watu hao bado hali yake ni
mbaya japo kuwa kuna dalili za kuweza hata kufumbua macho.
“Mlinzi wa Kanisa la Kihesa aliyejeruhiwa na kuletwa hapa hospitalini
bado hali yake ni mbaya na tumegundua kuwa alivunjika mfupa wa
kichwani kwa hiyo tunaendelea kufanya utaratibu wa kuutoa. Ila kwa leo
amekuwa na dalili za kufumbua macho kwa hiyo tunafanya jitihada za
kumpa huduma zaidi” alisema Dk. Faustine.
…………………………………….. Mwisho ……………………………
Subscribe to:
Posts (Atom)




